Monday, September 2, 2013

KILICHOJIRI KATIKA SERENGETI FIESTA MTWARA .

Ni shangwe za kutosha usiku huu ndani uwanja wa Nangwanda Sijaona mkoani Mtwara.

Msanii aliyeibuka kwa kasi hivi sasa katika muziki wa Bongofleva,aitwaye Snura akionesha staili ya Kuvurugwa jukwaani.

Add caption

Baadhi ya Wakazi wa mkoa wa Mtwara na vitongozji vyake wakiwa wamejitokeza kwa wingi kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2013,ndani ya uwanja wa Nangwanda Sijaona.

Anaitwa Dj Mully B akionesha umahiri wake wa kukamua mangoma mbele ya maelfu ya wakazi wa mji wa Mtwara waliojitokeza kwa wingi kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2013.

Mashabiki wa tamasha la burudani la Serengeti Fiesta 2013 wakifuatilia kwa makini yanayojiri kwenye tamasha hilo usiku huu ndani ya uwanja wa Nangwanda Sijaona mkoani Mtwara,ambapo wakazi wa mkoa huu kwa mara ya kwanza walishuhudia live tamasha hili ambalo hufanyika mara moja kwa mwaka.

Wakishangweka safi kabisa.

Ni burudani ya kutosha kabisa usiku huu ndani ya tamasha la serengeti fiesta ambapo maelfu ya watu wamejitokeza kuburudika ndani ya uwanaj wa Nangwanda Sijaona mkoani Mtwara.

Anaitwa Linah kutoka nyumba ya vipaji ya THT,akiimba jukwaani mbele ya umati wa wakazi wa Mtwara waliojitokeza usiku huu kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2013.

Kijana mdomo,lakini anaonekana kuja kwa kasi kabisa katika anga ya muziki wa kizazi kipya,hasa hip hop,aitwa kwa jina la kisanii Young Killer kutoka jijini Mwanza,akitumbuiza usiku huu mkoani Mtwara kwenye tamasha la Serengeti fiesta 2013.

No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...