Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Prof. Anna Tibaijuka akiwasalimia wakazi wa kata ya Bunju na Wazo mara baada ya kuwasili katika eneo hilo kwa lengo la kuzungumza nao ili kutafuta suluhisho la kudumu la mgogoro wa ardhi kati yao na kiwanda cha Saruji cha Twiga jana jioni.Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Prof. Anna Tibaijuka akiongea katika mkutano wa hadhara na maelfu ya wakazi wa kata ya Wazo na Bunju waliojitokeza kufuatilia maendeleo ya mgogoro wa ardhi kati yao na Kiwanda cha Twiga Cement ambapo pamoja na mambo mengine amewahakikishia wakazi hao kuwa mgogoro huo utapatiwa ufumbuzi wa kudumu na kuwaomba kutoa ushirikiano kwakeDiwani wa eneo la Bunju na Wazo Sharif Exavery Majisafi akiongea na wananchi kabla ya kumkaribisha Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Prof. Anna Tibaijuka kuzungumza nao.Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Prof. Anna Tibaijuka (kulia) akiongea na Mkurugenzi mtendaji wa kiwanda cha Saruji cha Twiga (Twiga Cement) Bw.Pascal Lessoinne (kushoto) mara baada ya mkurugenzi huyo kutoa taarifa fupi ya maendeleo ya kiwanda hicho na hali ya mvutano wa muda mrefu wa umiliki wa maeneo baina ya wakazi wa kata za Bunju na Wazo jijini Dar es salaam. |
Wednesday, December 5, 2012
WAKAZI WA KATA YA BUNJU NA WAZO WAFURAHIA WAZIRI WA ARDHI PROF. ANNA TIBAIJUKA KUINGILIA KATI MGOGORO WAO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment