Gari lililopata ajali la Rav 4 T 770 BNP eneo la Tanzangozi, Iringa
lililokua likiendeshwa na Bw. Ezekiel Mwaiteleke(Marehemu) majira ya saa
sita na nusu mchana na kusababisha vifo vya watu watano wa familia moja
papo hapo December 4, 2012
Baadhi ya kina mama wasamaria wema wa Tanzangozi Iringa wakijaribu
kumpepelea mmoja ya majeruhi wa ajali iliyotokea December 4, 2012 huko
Tanangozi, Iringa likihusisha Toyota Rav 4 T 770 BMP lililoingia nyuma
ya Trailer T 566 BNQ ambapo watu watano wa familia moja waliokua
wakitokea Dar kwenda Mbeya walifariki papo hapo
Gari aina ya Scania lenye cabin # T 840 BST likiwa na Trailer # T 566
BNQ likiwa limegongwa kwa nyuma na Toyota Rav 4 T 770 BNP huko
Tanangozi, Iringa na kusababisha vifo vya watu watano wa familia moja
papo hapo
Watu sita wamefariki dunia katika ajali mbaya
ya gari iliyotokea mkoa wa Iringa mapema siku ya jumatano
Ajali hiyo imetokea
katika eneo la Tanangozi wilaya ya Iringa kwenye kizuizi cha barabara cha
mafundi wa kutengeneza barabara kuu ya Iringa -Mafinga mkoani Iringa mida ya
saa nane mchana
Kwa mujibu wa mashuda
wa tukio hilo chanzo cha ajali hiyo ni dereva wa gari dogo aina ya Rav 4 lenye
namba za usajili T 770 BMP kuliparamia lori lenye tela kwa nyuma.
Katika ajali hiyo
abiria wote wanne akiwemo baba na mama wa watoto wawili waliokuwemo katika gari
hiyo wamefariki papo hapo
Majina ya waliokufa
ni pamoja na Ezekiel Mwaiteleke ambaye ni dereva wa gari hilo na baba wa
familia hiyo ,mkewe Grace Mwaiteleke ,mtoto Kelvin Mwaiteleke (2),Happy
Mwandike na mfanyakazi wao wa ndani aliyefahamika kwa jina la Linda Ezekiel
huku majeruhi katika ajali hiyo ni mmoja na amekimbizwa Hospital ya mkoa wa
Iringa.
|
No comments:
Post a Comment