Tuesday, June 26, 2012

 ZAIDI YA WATU 400 WANASA KWENYE MAPOROMOKO YA UDONGO  MASHARIKI MWA NCHI YA UGANDA

Taarifa kutoka nchini Uganda zinaeleza kuwa, shughuli za uokoaji zinaendelea katika eneo la mashariki mwa nchi hiyo ambako vijiji vitatu vimedaiwa kufunikwa na udongo, kufuatia maporomoka yaliyolikumkumba eneo la Bududa nchini humo 

Shirika la msalaba mwekundu nchini Uganda limethibitisha  kuwa zaidi ya watu kumi na wanane wamefariki dunia katika maporomoko hayo.wakati shughuliza kuwatafuta mamia ya watu walionasa zikiendelea 
Baadhi ya wananchi wa Uganda wakiwa sehemu ya maporomoko
 Vyombo vya habari nchini vimeripoti kuwa, watu wanaokadiriwa kufikia 450 hawajulikani walipo baada ya kutokea maporomoko ya udongo ya mfululizo ambayo yamefunika vijiji vyote vya maeneo ya milima ya Gugisu  na kuwaacha wakazi wa eneo hilo wakiwa katika hali ya taharuki 

 ijiji visivyopungua 11 vimefunikwa na matope na majabali mazito na hivyo kukumbushia maporomoko mengine ya udongo yaliyoyakumba maeneo hayo mwezi Machi 2010 na Agosti mwaka jana.

Mwaka 2010, maporomoko mengine ya ardhi yalitokea katika wilaya hiyo ya Bududa, na kuwauza zaidi ya watu mia tatu.

Maporomoko hayo ya udongo yadaiwa kutokea  kufuatia kunyesha kwa mvua kubwa

Eneo hilo linazungukwa na miinuko pamoja na mabonde, kando kando ya mlima Elgon, na hupokea mvua kubwa katika msimu wa masika.

baadhi ya nyumba zilizokumbwa na maporomoko hayo




Serikali ya Uganda imekuwa ikiwaimewashauri wakazi katika maeneo hayo kuhamia maeneo salama lakini wengi wamekataa kufanya hivyo wakihofia kupoteza mashamba yao yenye rotuba.

wananchi wa uganda katika eneo la maporomoko huko wilaya ya Baduda
Hata hivyo  Serikali ya Uganda inatarajiwa kutoa taarifa kamili kuhusu janga hilo huku ikisema kuwa itahakikisha kuwa familia zilizoathirika zinapata msaada wa kutosha''

No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...