MIONZI ya simu za mkononi inaweza kuathiri maendeleo ya
ubongo wa watoto walioko tumboni mwa mama zao, utafiti umeeleza.Utafiti huo
umetaja madhara mengine ya mionzi ya simu za mkononi kuwa ni uharibifu wa
manii, mimba, kupungua kwa nguvu za kiume, kupoteza kumbukumbu na kuzaa watoto
watukutu.
Pia
umeeleza kuwa matumizi kupita kiasi ya simu hizo, husababisha mtindio wa ubongo
na upungufu wa udadisi kwa watoto tangu udogo wao.
Hata hivyo, utafiti huo
uliofanywa na Shule ya Tiba na Dawa ya Chuo Kikuu cha Yale, Marekani na
kuripotiwa na Gazeti la The Telegraph la Uingereza, umepingwa na watafiti
wengine, wakisema haujakidhi baadhi ya vigezo ili kuuthibitisha.
Kiongozi wa jopo la utafiti huo, Profesa Hugh Taylor alisema utafiti huo
ulioanzia kwa panya, baadaye ulithibitika kwa binadamu.
Profesa Taylor ambaye pia ni Mkuu wa Idara ya Uzazi, Magonjwa ya Wanawake na
Sayansi ya Uzazi, alisema: “Tulikuwa na panya wenye mimba katika maboksi na
tuliwawekea simu juu ya vichwa vyao.
Panya tuliokuwa tumewaweka katika bwawa lile, nusu yao walikuwa
wazima na nusu yao walikufa. Panya waliokuwa hai tuliwaacha wajifungue na baada
ya kujifungua, tukaanza kutafiti watoto wao.”
“Panya ambao hawakuwa karibu na simu za mikononi walionekana kuwa werevu.
Kumbukumbu zao hazikupungua ikilinganishwa na panya walioathiriwa na mionzi ya
simu za mikononi ambao katika vipimo vya awali wakiwa tumboni, walionekana
kuhangaika.”
“Panya hao wenye mimba waliowekwa kwa siku 17 katika boksi hilo na simu kupigwa
mfululizo juu ya vichwa vyao, walizaa watoto watukutu na waliokosa kumbukumbu.”
Aliongeza: “Matokeo hayo yanaweza kutokea kwa binadamu pia. Mjamzito anayetumia
simu ya mkononi muda mwingi, anaweza pia kuzaa taahira.”
Utafiti huo umebaini kuwa kati ya asilimia tatu na saba ya watoto wenye umri wa
kwenda shule, wana tatizo la utukutu linaloweza pia kuathiri maendeleo yao
kitaaluma.
Alisema kiwango hicho kimekuwa kikiongezeka kwa asilimia tatu
kila mwaka tangu mwaka 1997.
|
No comments:
Post a Comment