Kesi ya mauaji ya marehemu Steven Kanumba inayomkabili movie star waTanzania Elizabeth Michael (Lulu) imeendelea kutajwa katika mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam huku suala la umri wa mshitakiwa huyo likiendelea kuwekwa kiporo.
Mbele
ya hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu AUGUSTINA MMBANDO,
Wakili wa Serikali KENNETH SEKWAO amesema upelelezi bado haujakamilika na kwa
sasa ipo katika hatua ya kutajwa.
Mapema
baada ya LULU kufunguliwa mashitaka ya mauaji ya msanii mwenzake STEVEN KANUMBA
April mwaka huu, mawakili wanaomtetea waliwasilisha hoja ya kupinga umri wa
mshitakiwa huyo na kutaka achukuliwe kama mkosaji mtoto kutokana na umri wake
kuwa chini ya miaka 18 hali iliyolazimu suala hilo kupelekwa Mahakama Kuu ya
Tanzania iliyoamua kulirejesha jambo hilo kwenye mahakama ya Kisutu.
Pamoja
na kurejeshwa kwa suala hilo katika mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu kumekuwa na
ukimya wa muda sasa, kesi ya LULU imeahirishwa mpaka Disemba 17 mwaka huu
ambapo itakwenda kwaajili ya kutajwa.
No comments:
Post a Comment