Sehemu ya ukuta uliobomoka |
Mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya sekondari Kwakilosa katika Manispaa ya Iringa Daniel Yona (15) amefariki dunia baada ya kuaungukiwa na ukuta wa uwanja wa Samora wakati akijaribu kupita mlango wa panya ili kwenda kushuhudia tamasha hilo la Mtikisiko 2012.
Tukio hilo lilitokea
usiku wa kuamkia Desemba 2 mwaka huu wakati wapenda burudani katika mkoa wa
Iringa walipofika katika uwanja huo kushuhudia onyesho kubwa la Mtikisiko 2012
ambalo lilikuwa limepambwa na wasanii mbali mbali wakiongozwa na mkongwe Juma
Nature na Profesa J.
Wakielezea
kilichomkuta mwanafunzi huyo baada ya mashuhuda walisema kuwa mwanafunzi huyo
na wenzake waliacha kupita katika mlango wa kawaida kwa kulipia kiingilio
halali kilichowekwa na badala yake aliamua kupita gizani na kupanda ukuta huo
wa uwanja wa Samora ili kuweza kuingia ndani ya uwanja huo kuona tamasha la
Mtikisiko.
Sehemu ya ukuta iliyobomoko na kusababishaa kifo cha mwanafunzi mmoja |
"Ujue hapa
vijana wa kihuni kutoka Kitanzini walikuwa wamejipanga hapa na kufanya ufisadi
wa kuwatoza watu kiingilio bila wahusika wa Tamasha hilo kujua kinachoendelea
.....hivyo hata huyo mwanafunzi alikuwa ni mmoja kati ya wavamizi wa Tamasha
hilo kwa kupita njia ya panya ili kuingia ndani ya uwanja huo" alisema
mmoja wa mashuda mbaye hakutaka jina lake litajwe
No comments:
Post a Comment