Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akipokea maelezo ya shamba
darasa kutoka Afisa Ugani Kata ya Matanga Ndugu Edith Shirima leo
alipoanza ziara yake Mkoani Rukwa kwa kuanzia katika kata hiyo. Kulia ni
Afisa kilimo Manispaa ya Sumbawanga Ndugu George Lupilya, Kaimu Katibu
Tawala Wilaya ya Sumbawanga. Kushoto ni Katibu wa Mkuu huyo Mkoa Frank
Mateni.
Shamba darasa katika kata ya Matanga kijiji cha matanga linalomilikiwa
na Mkulima mdogo Bibi Paschalia Ntinda. Mbolea ya kupandia iliyotumika
ni Minjingu Mazao.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa akisalimiana na Bibi Paschalia Ntinda amabaye ni mmiliki wa shamba darasa hilo.
Mkuu
wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya kushoto akisalimiana na
wananchi wakulima katika kata ya kasense leo alipoenda kukagua mashamba
darasa katika kata hiyo. Kata ya Kasense ipo katika Manispaa ya
Sumbawanga.
|
No comments:
Post a Comment