Monday, September 24, 2012



VIJANA WAAFRIKA WAASWA KUWA CHACHU YA MAENDELEO 
MEYA WA ILALA JERRY SILAA AKIWA NA KIONGOZI WA UJUMBE WA MSUMBIJI LOPEZ TEMBE NDELANA
Vijana katika nchi za Afrika wameaswa kuwa chachu ya mabadiliko yatakayosaidia kuleta maendeleo endelevu kwa ustawi wa wananchi wao

Ushauri huo umetolewa na kaimu katibu mkuu wa chama cha Mapinduzi ccm ambaye pia ni meya wa manispaa ya Ilala na mjumbe wa halmashauri kuu ya chama hicho Jerry Silaa wakati akiwapokea vijana 56 wanachama wa chama kinachotwala nchini Msumbiji cha FRELIMO waliokuja nchini ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 tangu chama hicho kianzishwe


Kaimu katibu mkuu huyo amesema vijana wa nchi za Afrika wanao wajibu wa kuhakikisha wanasaidia harakati za serikali zao katika kuwaletea wananchi maendeleo kwa kufanya kazi kwa bidii na kushiriki shughuli za vyama zenye lengo la kuleta umoja na mshikamano

Kwa upande wake kiongozi wa msafara huo wa vijana 56 kutoka mikoa yote nchini Msumbiji balozi Lopez Tembe Ndelana ambaye  ni mmoja wa waasisi wa vuguvugu la uhuru wan chi hiyo aliyeshiriki katika harakati hizo zilizoanzi ahapa nchini amewashukuru watanzania ambao walishirikiana na wananchi wa Msumbiji katika kujikomboa.


Msumbiji ilipata uhuru wake mwaka 1975 ikiwa chini ya chama cha FRELIMO ambacho kimefikisha miaka 50 jana Jumapili

No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...