Monday, September 24, 2012



BAADA YA SAKATA LA UBAGUZI WA RANGI HATMAYE JOHN TERRY AACHIA NGAZI KATIKA SOKA LA KIMATAIFA.

Baada ya FA kulishikia bango sakata la ubaguzi wa rangi hatmaye  John Terry, nahodha wa zamani wa timu ya taifa ya soka ya England, jana usiku ametangaza kustaafu kama mchezaji wa kimataifa.

Terry, ambaye ni mlinzi wa klabu ya Chelsea, na mwenye umri wa miaka 31, alitangazwa na mahakama ya Westminster mjini London mwezi Julai kwamba hana hatia ya kutumia matamshi ya ubaguzi wa rangi dhidi ya Anton Ferdinand, tukio ambalo lilifanyika katika mechi ya ligi kuu ya Premier.


Terry alimpigia simu meneja wa England, Roy Hodgson, kabla ya kuwasilisha wazi taarifa yake Jumapili jioni.

Alisema: “Kuendelea kufuatia mashtaka dhidi yangu wakati mahakama tayari imeshafanya uamuzi na kupata sina hatia….hayo hayanipi nafasi kutimiza wajibu wangu.”



No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...