Monday, September 24, 2012

MBUNGE WA VITI MAALUM KUSHOTO {CHADEMA} PHILIPA MTURANO
JAMII YATAKIWA KUWAUNGA MKONO WAALIMU KATIKA MALEZI.

Jamii imetakiwa kuwajibika kwa kuwaunga mkono walimu katika malezi ya wanafunzi ili waweze kupata mafanikio katika masomo.

Akizungumza wakati wa mahafali ya kidato cha NNE Shule ya sekondari Magnusi,Mbunge wa viti maalum kupitia tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Phillipa Mturano amesema walezi wamekuwa na tabia ya kuwaachia mzigo waalimu pekee.

Pia mbunge huyo amesisitiza wananchi kuchangia gharama za uendeshaji wa shule ili ziweze kukidhi mahitaji na malengo yaliyokusudiwa badala ya kuachia mzigo huo kwa serikali.

Katika hatua nyingine Bi Phillipa Mturano amewasihi  waalimu kutojihusisha na migomo bali wafuate taratibu za mazungumzo na serikali ili iweze kuwatimizia maslahi yao.


No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...