TETEMEKO LA ARDHI LASABABISHA VIFO VYA WATU 80 KUSINI
MWA CHINA
Tetemeko la ardhi lililotokea jana
mchana huko Yiliang, kusini mwa China limesababisha vifo vya watu 80 na wengine
zaidi ya laki 7.4 kuathiriwa.
Tetemeko hilo lenye nguvu ya 5.7
kwenye kipimo cha Richtar lilitokea katika sehemu ya mabonde yenye hali duni ya
maendeleo, na kuharibu vibaya miundo mbinu ya barabara na mawasiliano ya simu.
Hivyo kuchelewesha kazi ya kukusanya
habari kuhusu vifo na majeruhi pamoja na hasara za mali zilizosababishwa na
maafa hayo.
Waziri mkuu wa China amefika katika
sehemu hiyo kuongoza kazi ya uokoaji na kukabiliana na maafa.
No comments:
Post a Comment