Saturday, September 8, 2012



TOFAUTI KATI YA ALIYENACHO NA ASIYEKUWA NACHO NI CHANZO CHA VURUGU ZA MIGODINI NCHINI AFRICA YA KUSINI.


Watu wameanza kufikiria ni fundisho gani linalotakiwa kupata kutokana na tukio hilo pamoja na athari zake kwa siasa nchini Afrika Kusini. 

Wengi waliofanya mgomo ni wale wanaofanya kazi ya kupasua mwamba, ambayo ni kazi muhimu zaidi katika mgodi wa madini ya platinum, lakini pia ni kazi ngumu na hatari zaidi, kwani wachimba madini wanaweza kufa au kujeruhiwa kutokana na maporomoko ya udongo au mwamba unaweza kuwaangukia wakati wowote.

Wachimba madini wanatarajia kuwa na maisha bora na mazuri, lakini hali ni tofauti, kwani mishahara yao inayoanzia dola 500 hadi 660, inawafanya wawe na hali ngumu ya kimaisha katika nyumba walizopewa na kampuni wanazofanyia kazi. 

Matatizo mengi yanawakabili, kama vile ukosefu wa maji safi na salama ya kunywa, nymba bora za kuishi  pamoja na kupanda kwa mfululizo kwa bei za bidhaa nchini Afrika Kusini. 

Mbali na kampuni ya Lonmin kukataa kutimiza madai yao ya kuongezewa mishahara, kinachowakasirisha wachimba madini hao ni pengo kubwa kati ya matarjiri na maskini. 


Afrika Kusini ni nchi iliyoendelea zaidi katika bara la Afrika, lakini nchi hiyo pia inakabiliwa na matatizo mbalimbali, ikiwemo mfumuko mkubwa wa bei, robo ya wananchi wake hawana ajira, na pengo kubwa kati ya matarjiri na maskini.

Wastani wa pato la taifa GDP nchini Afrika Kusini limefikia dola 8,000 za kimarekani, lakini karibu asilimia 40 ya watu wake wanaishi kwa chini ya dola 3 kwa siku. 

Pengo hilo kubwa linaonekana zaidi katika sekta ya madini.

 Chama cha wafanyakazi wa nigodini ni mwenza wa muda mrefu wa chama tawala, ANC, na mwenyekiti wa zamani wa chama hicho cha wafanyakazi Cyril Ramaphosa ni mtu maarufu sana ndani ya ANC, Ramaphosa pia ni mjumbe wa bodi ya kampuni ya Lonmin, na ni miongoni mwa watu matajiri zaidi nchini Afrika Kusini. 

Wachimba madini wanaofanya kazi ya kupasua miamba wanalalamika kuwa, chama cha wafanyakazi cha sekta ya madini kinapuuza madai yao, ndiyo maana wengi wamejiunga na shirikisho la vyama vya wafanyakazi vya sekta za madini na ujenzi, ambalo liliongoza mgomo katika mgodi wa Marikana. 

Kufuatia tukio hilo, thamani ya Rand ya Afrika Kusini ilipungua kwa asilimia 1.5 ndani ya siku moja. 

Katika wiki mbili zilizofuata, wawekezaji wa nchi za nje waliuza dhamana za Afrika Kusini zenye thamani ya dola milioni 373. Nchi za  China na Brazil, Afrika Kusini imefanikiwa kuvutia mitaji kutoka nchi za nje. Lakini baada ya tukio hilo la umwagaji damu, wawekezaji wanachukua tahadhari kubwa kabla ya kuamua kuwekeza nchini Afrika Kusini.

No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...