Friday, September 7, 2012


            SIMU SILAHA TOSHA YA KUKAMATA MWIZI GHANA 

Mvumbuzi wa huduma ya "Hei Julor", Herman Chinery-Hesse wa Ghana.
Herman Chinery-Hesse Mvumbuzi wa programme
 Mvuumbuzi wa programu hii ya Kighana Herman Chinery-Hesse alitaka kuchukua hatua dhidi ya matukio ya ujambazi wa kutumia silaha mjini Accra. Ndivyo alivyokuja na programu hii ya "Hei Julor" au "Ewe mwizi" kwa lugha ya wenyeji wa mji huo.

"Hei Julor" ni programu ya mfumo wa usalama inayotumiwa katika simu ambapo mtu anaweza kutuma ujumbe mtupu kutoka kwenye simu zaidi ya tano zilizosajiliwa katika eneo, pale makaazi ya mtu au biashara yanapovamiwa.

Hatua hii inasababisha kutumwa kikosi cha waokoaji kutoka kampuni binafsi ya ulinzi, na wakati huo huo watu wengine kumi wakiwemo majirani na marafiki wanapata ujumbe huo na wanaweza kufika haraka nyumbani kwa mhusika ili kumsaidia.

Huduma hii ya Hei Julor ilizinduliwa chini ya mwaka moja nyuma, wakati wa vuguvugu la mageuzi katika mataifa ya kiarabu na wakati ambapo maandamano ya vrugu yalikuwa yanafanyika nchini Uingereza.

Herman Chinery-Hesse akiwa ofisini wake.

Katika matukio yote mawili, teknolojia ya simu za mkononi kama vile ujumbe wa Blackberry au BBM ulikuwa ukitumika kuratibu shughuli. Chinery-hesse, ambaye amepewa jina la baba wa teknolojia barani Afrika anakumbuka jinsi yeye na marafiki zake walivyokuja na wazo la "Hei Julor."

"Tulikuwa tunafuatilia maandamano katika nchi za kiarabu and nchini Uingereza kupitia redio mchana moja na ikatujia akilini kuwa walikuwa wakitumia BBM kuratibu maandamano hayo. laazima itakuwa na manufaa makubwa kwa jamii yetu, katika utamaduni wetu au nchi yetu. Na kwa sababu hiyo, tulikuja na wazo la "Hei Julor."

Haikuwachukulia muda Chinery-Hesse na marafiki zake wanaofanya kazi katika kampuni ya programu za kompyuta ya "Softribe" kuweka mawazo hayo katika vitendo.

"Tumekuwa wataalamu kwa vile hii ndiyo kazi tunayoifanya kazini kwetu, kwa hiyo tulikuwa na vifa vyote vinavyohitajika. Tulikaa ofisini, tukamualika kila moja kuhudhuria kikao na kujadili namna ya kuja na huduma ambayo kila moja angeweza kuipata kwa bei nafuu na kuizuia Ghana kuwa taifa la wahalifu." Anasema Chinery-Hesse.

No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...