Tuesday, September 25, 2012


Maadhimisho ya Siku ya Bahari Duniani katika Viwanja vya Karimjee kuanzia tahere 26 - 27 Sept. 2012

Kila mwaka Shirika la Kimataifa la Bahari (IMO) huadhimisha siku ya Bahari Duniani (World Maritime Day). 

Kaulimbiu ya Siku ya Bahari kwa mwaka huu ni “IMO: Miaka 100 baada ya Titanic”. . Kauli mbiu hii inalenga katika kudhibiti ajali zinazohusisha vyombo vya usafiri wa majini. 

Katika kuadhimisha siku hiyo hapa Tanzania, shughuli mbalimbali za uelimishaji umma kuhusu usalama wa usafiri majini zitafanyika kama sehemu ya maadhimisho ambapo kutakuwa na maonesho ya shughuli zinazofanywa na taasisi zinazojihusisha na usafiri wa majini yatakayofanyika kuanzia tarehe 26 – 27 Septemba, 2012 katika Viwanja vya Karimjee.
Taasisi na makampuni yatakayoshiriki maonesho ni pamoja na Wizara ya Uchukuzi, Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA), Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Chuo cha Bahari cha Dar es Salaam(DMI), Kilimanjaro Marine Services na Songoro Marine Services.

Aidha SUMATRA imeandaa mkutano wa wadau ambapo itatumia fursa hiyo kuwasilisha kwa wadau rasimu za kanuni za usalama wa usafiri wa majini. Mkutano huo utafanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Karimjee tarehe 27 Septemba, 2012 kuanzia saa 3.30 asubuhi.

Maadhimisho ya Siku ya Bahari yanatarajiwa kuzinduliwa rasmi na Waziri wa Uchukuzi, Mheshimiwa Dk Harrison Mwakyembe (MB) tarehe 25 Septemba, 2012.

Wadau na wananchi wote mnakaribishwa katika viwanja vya Karimjee ili kupata elimu na kujionea juhudi za Serikali na baadhi ya makampuni ya usafiri wa majini katika kuimarisha usalama wa vyombo vya majini.

No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...