Wednesday, September 12, 2012



JE DHIMA YA KUWA NA MFUMO WA VYAMA VINGI TANZANIA INAIELEWEKA?
 http://3.bp.blogspot.com/-ezDFVaIsNVU/T__P0km4n1I/AAAAAAAAL4k/bY5rBClZMzo/s640/Katuni+Tendwa.jpg




Tangu mwaka 1992 tanzania ilipoanza rasmi mfumo wa vyama vingi vya siasa, hali imekuwa ikizidi kubadilika siku hadi siku na hii inatokana na ukweli kwamba mwitikio wa wananchi umekuwa ukizidi kukua kila iitwapo leo.

Tangu chaguzi ya kwanza ya vyama vingi mwaka 1995, kumekuwa na ripoti mbalimbali za ukiukwaji wa haki za binadamu ambapo rapsha rapsha za hapa na pale ambazo zimekuwa zikifuatana na milindimo ya risasi imekuwa ikisikika,

Nje kidogo ya kongamano lililoandaliwa na muungano wa asasi za kirai nchini ambalo limefanyika katika viwanja ya mtandao wa kijinsia Tanzania TGNP, blog hii imepata fursa ya kuzungumza na baadhi ya wadau pamoja na wasomi ambao kwanza wanazungumzi milindimo hii ya risasi katika nchi inayotajwa kama ya kidemocrasia

Wamesema kuwa ni vema watawala wakavitumia vyombo vya ulinzi na usalama kuwa kuhakikisha vinatimiza wajibu wao wa kulinda usalama wa nchi na si kuwa vyanzo vya kubomoa amani ya nchini,

Lakini katika nchi ya kidemocrasia kama Tanzania ni yapi yanapaswa kuzingatiwa ilikuilinda democrasia iliyopo, wanasheria Haloid sungusia na Albanie   marcos wanazungumza.

Katika duru za kisiasa kwa upande wa kimataifa Tanzania imekuwa ikijengea heshima kwa kutajwa kama nchi inayojali na kuheshimu misingi ya kidemocrasia.

No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...