Wednesday, September 12, 2012



       NCHIMBI AKUMBANA NA KADHIA KWENYE MAANDAMANO.


Maaandamano ya yaliyowajumuisha kwa pamaoja waandishi wakongwe na chipukizi nchini  yamefanyika kwa amani na utulivu  huku waandishi  wakitakiwa kudumisha umoja na mshikamano   


 Maandamano hayo yameanzia  kituo cha  televisheni cha Channel Ten alichokuwa akifanyia kazi Daudi Mwangosi hadi viwanja  vya  jangwani huku wanahabari wakivalia  nguo nyeusi ishara  ya kuomboleza kifo cha mwenzao.



Baada ya kufika katika viwanja vya Jangwan waziri wa Mambo ya Ndani, Emmanuel Nchimbi, amekambana na fedhea  ambayo haikutarajia wakati alipotimuliwa  katika maandamano hayo kwa   madai  kuwa hakuna kiongozi yoyote wa serikali aliyealikwa

Wakati wakiwa wamebeba mabango yenye ujumbe tofauti, walipofika mwisho wa maandamano yao walipigwa na butwaa baada ya kumkuta Waziri Nchimbi akiwa wa kwanza kufika katika eneo hilo tayari kupokea maandamano.


Wakati Nchimbi akijiandaa kuanza kuzungumza mbele ya wanahabari, upinzani mkali ulizuka kwa waandishi dhidi ya kiongozi huyo wa serikali wakitaka aondoke mahala hapo kwani maandamano hayo yalikuwa hayamuhusu.

‘Atokee....  nchimbi …aondokee.... nchimbi , hatumtakiiii.... nani kamleta hapa?" yalikuwa ni baadhi ya maneno yaliyokuwa wakitolewa kwa sauti kubwa kupinga uwapo wa kiongozi huo

Waziri wa mambo ya ndani Emmanuel Nchimbi akilazimika kuondoka kwenye maandamano hayo

Mwandishi wa habari mkongwe, ambaye pia ni mwanasheria, Nyaronyo Kicheere, alisogea mbele ya umati wa waandishi na kusimama jirani na alipokuwapo waziri Nchimbi na kusema: "Tumeambiwa tunakuja hapa kwa ajili ya mkutano wa waandishi wa habari na utapokewa na jukwaa la wahariri, inakuwaje tupokewe na mtu mwingine. Hatumhitaji mtu mwingine hapa, aondoke."

Baada ya kauli hiyo, waziri Nchimbi aliondoka mahala hapo na kuzua shangwe kubwa kwa waandishi ambao pia walimsindikiza kwa kumzomea mpaka alipoingia katika gari lake la wizara. Hakuja na gari lake la waziri.



Wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari walizungumza na kukemea mauaji hayo na bila ya kinyama  yanayofanywa  nchini huku wakitaka waliomuua mwandishi huyo  wote wachukuliwe hatua za kisheria.


Maandamano hayo pia yamefanyika katika mikoa mingine nchini isipokua mkoa ya Mara na Arusha.




No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...