Tuesday, September 18, 2012



MANISPAA YA KINONDONI INADAIWA KIASI CHA SHILINGI  BILIONI  8 KUFUATIA KUVUNJA MAKAZI  YA WANANCHI BILA KUFUATA TARATIBU ZA KISHERIA 

Manispaa ya  kinondoni  jiji Dar es salaam inadaiwa  kiasi cha shilingi bilioni nane na wakazi wa maeneo hayo kufuatia kuvunjwa kwa maeneo yao bila ya kufuata utaratibu kutoka serikalini 

Hayo yamesemwa September 18 mwaka  huu   na mstahik Meya wa manispaa hiyo  Bw Yusuph Mwenda alipokuwa akijibu hoja mbalimbali zilizokuwa zikitolewa na madiwani wa manispaa hiyo  katika kikao chao cha kawaida cha kujadili mambo mbalimali ikiwemo suala la uvamizi wa maeneo ya wazi
Yusuph Mwenda Mstahik meya Manispaa ya Kinondoni


Bw. Mwenda amesema kiasi hicho cha fedha kinachodaiwa kimesababishwa na baadhi ya watendaji wa kata na manispaa kuvamia maeneo ya wakazi bila ya kufuata taratibukutoka ngazi za juua
Amesema kitendo hicho  kimemsikitisha  na watendaji hao wanapaswa kuwajibishwa ili iwe fundisho kwa watendaji wengine wenye tabia kama hiyo .

Hivyo meya huyo amefafanua kwamba  bado kumekuwepo na tabia ya baadhi ya watu  wanaoendelea kujimilikisha kiholela maeneo ya serikali ambayo ni maeneo ya wazi  kinyume cha sheria ,hivyo amewataka watu wa namna hiyo waliovamia maeneo ya Kimara, Mwagwepande, Magomeni Sinza  kuhama mara moja

Kwa upande wake mkurugenzi wa manispaa hiyo Bw .Frutunatus Fuema amesema mwishoni mwa mwaka huu manispaa hiyo itachukuwa hatua,ya kuweka alama katika maeneo yaliyotengwa  ili serikali iweze kujua maeneo yake.

Zoezi la bomboa bomoa manispaa ya Kinondoni



No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...