Wednesday, September 19, 2012



 
       
          VIKAO VYA CCM NEC KUANZA HIVI KARIBUNI

Kikao cha halimashauri kuu ya Chama Cha Mapinduzi  NEC  kinatarajia kufanyika kuanzia September 24 mwaka huu mkoani Dodoma, kwa ajili ya kuteuwa majina ya wagombea waliojitokeza kugombea nafasi mbalimbali ndani ya chama hicho .

Akizungumza na waandishi wa habari  September 18  mwaka huu Katibu wa NEC itikadi na uenezi  bwana Nape Mosses  Nauye amesema kikao hicho kitakaa baada ya kamati kuu kukutana November 22 na 23 mwaka huu.

Amesema September 19 na 20vikao vya Sekretarieti vitaanza lengo likiwa ni kupitisha majina ya wagombea  kwa kuzingatia alama walizoekea katika vikao vilivyokwisha fanyika.

Kikao hicho cha sekretarieti kikimalizika,watapeleka mapendekezo yao katika kikao cha kamati ya  maadili ambacho kinatatarajiwa kukutana September 21

Katibu huyo amebainisha kuwa vikao vyote hivyo vitakuwa  ni kwaajili ya kuchuja majina  kuanzia kwenye jumuiya  katika ngazi ya kitaifa wenyeviti na makamu wenyeviti katika ngazi za mkoa na wilaya na kwamba NEC itakapokutana ndiyo itakayoteuwa majina ya wagombea na baada ya hao ratima ya uchaguzi itatolewa.

Amesema Viongozi Wakuu Wakitaifa Wanatarajiwa Kukutana  Mwishoni Mwa Mwezi November Kwa Ajili Ya Uchaguzi Nafasi Ya Mwenyekiti Makamu  Mwenyekiti

Katika hatua nyingine  bwana Nape amefafua katika kikao hicho kuhusu uwepo wa mtu  asiyejulikana anayetumia jina lake  kuwarubuni baadhi ya wagombea na kuwaomba fedha  na kusema  mtu huyo amesajili account yake kwa Jina lake hivyo kuwaomba wagomea na watanzania kwa ujumla  kutambua kwamba mtu huyo ni tapeli na kwamba hakuna jina la mtu yoyote litakalopitishwa kwa njia ya rushwa.

No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...