Friday, September 7, 2012


    OBAMA AKUBALI UTEUZI WA CHAMA CHAKE CHA DEMOCRATIC

Rais wa Marekani Barack Obama amekubali uteuzi wa chama chake, Democratic, kugombea muhula wa pili wa Urais. 

Katika hotuba yake Obama amewaomba raia wa Marekani kuwa na subira huku akisema itachukua muda kupata suluhisho kwa changamoto zinazoikabili nchi hiyo 

Rais Barack Obama wakati wa akiwahutumia wanachama wa chama chake

.

 Ilikuwa wakati wa hotuba yake kwenye kilele cha mkutano mkuu wa chama hicho, ambao umefanyika katika mji wa Charlotte, katika jimbo la North Caroline.

Akizungumza mbele ya wajumbe 6000 katika mkutano huo, Obama amesema katika uchaguzi wa mwezi Novemba ambao atakuwa akipambana na Mitt Romney wa chama cha Republican, wamarekani watakuwa  na nafasi kubwa ya kuamua  juu ya mielekeo miwili tofauti kwa Marekani.

Rais Obama Amekiri kwamba nchi yake inakabiliwa na changamoto  nyingi za a kiuchumi  kiuchumi, huku akasema changamoto hizo zinaweza kupatiwa ufumbuzi.

'Itachukua miaka michache mingine kuweza kuukwamua uchumi ambao umekuwa ukiporomoka kwa miongo kadhaa. Itahitaji juhudi za pamoja, kuwajibika kwa kila mmoja wetu, na ujasiri kama ule wa Rais Franklin Roosevelt wakati wa mgogoro mkubwa pekee kuliko huu wa sasa''. Amesema Obama.


Ikiwa imeasalia miezi miwili kabla ya kufanyika uchaguzi wa mwezi Novemba, Rais Obama na mpinzani wake Mitt Romney bado wako sambamba katika kura za maoni, wademocrats wanazinadi sera zao kuhusu masuala ya usalama, haki za wanawake na mashoga, uokozi wa sekta ya viwanda vya magari na kuuawa kwa Osama bin Laden kujaribu kumpa msukumo Rais Obama aweze kumpita mpinzani wake.

Rais Barack obama kulia ,kushoto ni rais wa zamani wa Marekani Bil ClintoN

Barack Obama ambaye kampeni zake zinamuonyesha kama mtu anayejali zaidi wamarekani wa kawaida na haki ya kila raia kutimiza ndoto yake, amehitimisha hotuba yake kwa kuwataka watu wenye maoni kama yake kumuunga mkono.

 Amesema, ''Kama una imani katika nchi ambayo inampa haki kila raia, na ambako watu wote wako sawa mbele ya sheria, basi, naomba kura yako katika uchaguzi wa mwezi Novemba''.

Maafisa wa chama cha Democrats wameuchukulia mkutano wao mkuu kuwa wa mafanikio makubwa, na ambao umeweza kuamsha hamasa ya wapiga kura.

No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...