Monday, September 10, 2012



KAMATI  KUU YA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA  MAENDELEO CHADEMA YATAKA VIONGOZI WA JESHI LA POLISI NCHINI WAWAJIBIKE 

Baada ya kukukutana na kujadili mambo mbali mbali ikiwemo mwenendo wa siasa hapa nchini pamoja na mauwaji ya raia  yaliyotokea hivi karibuni   hatmaye ,kwa kauli moja chama hicho kimwewataka  viongozi wa juu wa Jeshi la polisi  kuwajibika 

Chama hicho kimesema kuwa ikiwa vingozi hao watashindwa kuchukuwa  hatuo hiyo bas I ni vema raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania  Dr. Jakaya Mrisho Kikwete awawajibisha .

Freeman Mbowe Mwenyekiti CHADEMA

Katika hatua nyingine viongozi  hao wa CHADEMA pia wameazimia kutoshiriki shughuli zitakazosimamiwa na msajili wa vyama vya siasa nchini John Tendwa kufuatia kauli aliyoitoa hivi karibuni ya kufuta chama kinachosababisha  mauaji ,hatua ambayo imepingwa vikali na chama hicho .

 Chama hicho pia kinataka rais  kuunda tume ya kimahakama 
 itakayochunguza  vifo vinavyotokea katika mazingira  tete  kukamatwa na kufikishwa mahakamani kwa mkuu jeshi la polisi mkoa wa Iringa  Michael Kamuhanda ,Mkuuu  wa kikosi cha kutuliza ghasia  mkoa wa Morogoro  pamoja na maaskari waliomuua aliyekuwa mwandishi wa channel Ten  Daudi Mwangosi.

Maazimio mengine ni yaliyotolewa na chama hicho  ni pamoja na   kuwavua uanachama  madiwani wawili wa chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA mkoa wa Mwanza walioenenda kinyume na sheria na kanuni za chama hicho

No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...