Tuesday, December 4, 2012

MKAPA, ANNAN WAKANUSHA KUINGILIA MAMBO YA KENYA





Katibu Mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa, Kofi Annan na Rais Mustaafu wa Tanzania Benjamin Mkapa

Katibu Mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa, Kofi Annan na Rais Mustaafu wa Tanzania Benjamin Mkapa wamekanusha madai kwamba wanaingilia masuala ya ndani ya Kenya. 

Wawili hao wamesema hayo kwenye mkutano wao na waandishi wa habari mjini Nairobi.

Mkapa na Annan wako nchini Kenya kwa niaba ya Jopo la Shaksia Mashuhuri kufuatilia mkakati uliowekwa na serikali ya Kenya kuhakikisha uchaguzi mkuu unafanyika kwa njia ya uwazi. 

Mkapa amesema jukumu lao ni kuona makubaliano ya kitaifa ya amani ya mwaka 2008 yanatekelezwa ili kuepuka machafuko ya kisiasa baada ya uchaguzi mkuu ujao. 

Kofi Annan kwa upande wake amesema, Kenya ni nchi huru na wao ni marafiki tu wa nchi hiyo na wala hawana nia ya kuanisha mustakabali wake wa kisiasa. 

Wanasiasa kadhaa wamekuwa wakidai kwamba Annan na wenzake wamekuwa wakitoa matamshi yanayoonyesha kuwa, wanaingilia mambo ya ndani ya Kenya.

No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...