Wednesday, August 1, 2012


 HISTORIA YARAIS BASHAL AL ASSAD
Bashar Hafez al-Assad rais wa Syria  alizaliwa tarehe  11ya mwezi  Septemba  mwaka 1965, katika  miji wa Dameski  nchini  SYRIA 

Baba yake, Hafez al-Assad, alizaliwa katika familia maskini na ndie aliyefanikiwa kufufua tawi la chama cha kiarabu cha  ujamaa Ba'ath nchini syria ambapo baada ya mapinduzi ya mwaka 1970 alianza kuiongoza kama  rais wa nchi hiyo 

Ufanisi  na umakini  wa  Hafez al-Assad  katika historia ya syria  kama kiongozi ndio uliompajina la Simba katika  mataifa ya kiarabu .
Bashar al-Assad alipata elimu yake ya msingi na sekondari katika  shule yenye mchipuo wa lugha za Kiarabu-Kifaransa  ya al-Hurriya katika mji wa Damascus

mwaka 1982, alihitimu  shule ya sekondari na kwenda kusoma mafunzo ya  ufamasia na matibabu katika Chuo Kikuu. . cha Damascus .

 Mwaka 1988, Bashar al  Assad alihitimu kozi hiyo na  kuanza kufanya kazi kama daktari katika hospitali ya jeshiya , "Tishrin", iliyoko nje kidogo ya  mji wa Dameski

Miaka minne baadaye, alikwenda Uingereza  kuanza mafunzo yake  shahada ya uzamili kitengo cha  Ophthalmology katika Hospitali ya western Eye  sehemu ya  kundi la hospitali za kufundishia za  St Mary katika jiji la London 

Bashar  al assad wakati  huo alikuwa hana matarajio makubwa  yakuwa mwanasiasa ambapo kaka yake , Bassel al-Assad , alitarajiwa kama rais wa baadaye, lakini kamwe hakutangaza  dhamira hiyo
1994 Rais  Bashar,  alihitisha kikao cha na jeshi baaada ya  kifo cha kushtukiza cha kaka yake  Bassel wa kilichosababishwa na ajali ya gari
Muda mfupi baadae  baada ya kifo cha Bassel, Hafez Assa baba wa rais wa Syria  alimtangaza Bashar Al Assad kama mrithi wa wazi wa Utawala wake .
Rais Bashar Assad aliandaliwa utaratibu maalumu wa kutambulishwa uliokuwa katika awamu tatu kwanza alimpeleka jeshini na pili picha yake ilitambulishwa kwa Umma na tatu alikaimumadaraka kama kiongozi wa syria baada ya kifo cha baba yake mwaka 2000.
Baada ya kifo cha baba yake, mwaka 2000, Bashar aliteuliwa kiongozi wa chama cha Ba'ath na Jeshi, na alichaguliwa kuwa rais bila kupingwa katika bunge la nchgi hiyo kwa kupata asilimia (97.2% ya kura),
Sambamba na kazi yake ya kijeshi, Bashar alikuwa kushiriki katika masuala ya umma. Alipewa mamlaka kubwa  kama  mshauri wa kisiasa kwa Rais Hafez al-Assad, mkuu wa ofisi ya kupokea malalamiko ya rufaa ya wananchi, na pia aliongoza kampeni dhidi ya rushwa.

Tarehe 27 Mei 2007, Bashar kupitishwa kama rais kwa kipindi kingine cha miaka saba, pamoja na matokeo rasmi ya 97.6% ya kura katika kura ya maoni bila ya mgombea mwingine [28].
Kisiasa na kiuchumi, maisha ya watu wa Syria yamebadilika kidogo tangu mwaka 2000.
Katika mahusiano ya nje rais wa Syria bashal al AL Assad amekuwa na mhusiano ya karibu na mataifa ya China na Urusi kutokana na uekezaji mkubwa wa mafuta ndani y\a nchi yake  lakini pia uhusiano mdogo na uliotetereka kwa jumuiya ya nchi za kiarabu na mataifa ya Magharibi.
Kufuatia upepo wa mabadiliko katika mataifa ya kiarabu  ulioazia Tunisia  ,Serikali ya rais Bashar  AL ASSAD haikusalimika maandamano nchini Syria yalianza tarehe 26 Januari 2011.
Waandamanaji wito wa mageuzi ya kisiasa na wakitaka kuerjeshwa kwa  haki za kiraia, pamoja na kuondolewa kwa sheria ya hali ya hatari ambayo imedumu tangu mwaka 1963

No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...