Tuesday, October 23, 2012

UCHAGUZI MAREKANI

RAIS  OBAMA ANG'ARA DHIDI YA  MPINZANI WAKE KATIKA MDAHALO WA MWISHO KUELEKEA UCHAGUZI

 
Picture
BAADHI YA RAIA WA MAREKANI WAKIFUATILIA SERA ZA WAGOMBEA URAIS NCHINI HUMO.
Ilikuwa ni sehemu ya tatu naya mwisho ya midahalo ya wagombea urais nchini marekani kabla ya kufanyika kwa  uchaguzi mwezi November mwaka huu  huku kila mmoja akionekana kunadi sera zake ili kupata uungwaji mkono  kwa wapiga kura .

Katika   sehemu kubwa ya mdahalo wao wa muda wa saa moja na nusu ilikuwa juu ya sera ya nje ya Marekani  kuhusiana na Iraq,Afghanistan ,Libya,  china  Iran  na Mashariki ya Kati.

Romney alimlaumu Rais Obama kwa kushindwa kutoa uongozi unaofaa kwa dunia na kuruhusu amani mashariki ya kati kuvurugika. 

Mitt Romney akaanza kwa kumpongeza  Rais Obama kwa kumzima  Osama Bin Laden na kwa kuwakabili viongozi wa al-Qaeda, lakini Romney akaelezea kuwa Marekani haiwezi kuondokana na hatari hiyo kwa njia ya kuua pekee.

Ushindani wa kiuchumi na pamoja na kijeshi baina ya nchi ya marekani na China ,ni miongoni mwa mambo yaliyodadiliwa  huku wagombea wote wakionekana kuunga mkono ushirika wao na taifa hilo lapili kwa uchumi duniani, lakini Obama yeye akiongeza kuwa yafaa marekani ikawekeza kwenye elimu pamoja na tafiti ili ili kuendelea zaidi 

Mjadala huo uliofanyika katika chuo kikuu cha Boca Raton, haukuwa na ubishi kama mjadala wa pili wiki iliyopita ambapo rais Obama alijitokeza  kwa kujikaza kisabuni kuonyesha wapiga kura kuwa yeye  ndiye kiongozi anayestahili kuchaguliwa mwaka ujao.

Kura za maoni zilizotolewa punde baada ya kukamilika mjadala huo, zilionyesha kuwa rais Obama  ni mshindi.

FUATLIA SERA ZA  NJE ZA MAREKANI YOTE MDAHALO WA MWISHO HAPO JUU.

No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...