RWANDA YAENDELEA KUKANUSHA MADAI YA KUWAFADHILI WAASI WA DRC
Serikali ya Rwanda imeendelea kukanusha vikali tuhuma kuusu kuwafadhili
waasi wanaopambana na serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DR
wanaoendeleza mapambano mashariki mwa nchi hiyo
Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda amesema hayo
akiwa katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa UN na kusema uzushi na taarifa
ambazo zinaihusisha nchi hiyo kufadhili waasi wa DRC hazina ukweli wowote.
Waziri wa mambo ya nje wa Rwanda -Louise Mushikiwabo |
amesema serikali yake ipatiwe ushahidi
unaodhihirisha wao ndiyo vinara wa kuwahifadhi
waasi wanaopambana na serikaliya Kinshasa kutoka eneo la Mashariki.
Waasi wa DRC Congo. |
Mapambano ya mashariki mwa nchi ya Jamuhuri ya
demokrasia ya Congo dhidi ya waasi yamechangia adha nyingi kwa wakazi wa maeneo
hayo ikiwemo vifo,watu kuyakimbia makazi yao,kukosekana kwa utulivu na hivyo
watu kushindwa kuendelea na shughuli za uzalishaji.
Raia wa Congo DRC wakiyakimbia makazi yao kutokana na ghasia baina ya waasi na majshi ya serikal |
No comments:
Post a Comment