Thursday, October 25, 2012



KIONGOZI WA BAKWATA ARUSHA AJERUHIWA KWA BOMU.
ABDUL KARIM JONJO KATIBU WA BAKWATA -ARUSHA AKIELEZEA NAMNA ALIVYOJERUHIWA  .
 Taarifa kutoka mkoani arusha zinaeleza kuwa katibu wa BAKWATA mkoa huo amenussurika kufa baada ya kujeruhiwa  na mlipuko wa bomu unaodaiwa  kutekelezwa na watu wasiojulikana nyumbani kwake. 
ABDUL KARIM MARA AKIPATIWA MATIBABUBAKATIKA WODI YA MAJERUHI HOSPITALI YAMKOA WA ARUSHA
Abdulkarim Jonjo mwenye umri wa miaka 52 amelazwa katika hospitali ya mkoa huo ya Mount Meru akiendelea kupatiwa matibabu zaidi.

Akizungumzia tuiko hilo akiwa katitika wodi ya majeruhi amesema  majira ya saa 6 :30 usiku akiwa amelala alishtukia  kuona mwanga moto dorishani mwake na kusikia kishindo kikubwa cha cha mlipuko.

NYUMBA YA KIONGOZI HUYO ,SEHEMU YA DIRISHA LILIPORUSHWA BOMU HILO
Amesema alilazimika kuamka na kutazama   tukio hilo lakini kabla ya kufika alisikia kishindo kingine  kilichomjeruhi vibaya baada ya kurushwa ndani ya chumba chake.
KAMANDA WA POLISI MKOA WA ARUSHA LIBERATUS SABAS AKITAZAMA GANDA LA BOMU LINALODAIWA KURUSHWA KWENYE NYUMBA YA KIONGOZI HUYO


No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...