Sunday, October 21, 2012



DKT. HARISSON MWAKYEMBE KUSHGHULIKIA MAPENDEKEZO YA KAMATI ILIYOTEULIWA KUCHUNGUZA MADUDU KATIKA BANDARI YA DAR ES SALAAM.
WAZIRI MWAKYEMBE KULIA AKIPOKEA RIPOTI YA UCHUNGUZI KATIKA BANDARI YA DAR ES SALAAM KULIA NI MWENYEKITI WA KAMATI HIYO BERNARD MBAKILEKI {Picha na father kidevu}
 Waziri wa uchukuzi Dkt Harison Mwakyembe amesema , hadi kufikia desember mwaka huu atahakikisha wizara yake inatekezeleza mambo  yaliyopendekezwa kwenye  kamati ya kuchunguza utendaji  kazi wa  mamlaka ya  ya bandari nchini TPA ili kutoa sura mpya ya  kiutendaji 

Dkt. Mwakyembe ameyasema hayo jijini Dar es salaam mara  baada ya kupokea ripoti ya kamati hiyo hiyo ya watu saba aliyoiteuwa agosti 27 mwaka huu kuchunguza masuala mbalimbali katika bandari ya Dar es salaam

Amesema mamaka ya bandari Tanzania TPA ni miongoni mwa bandari kubwa elfu 36 barani afrika ambapo licha ya ukubwa na ukongwe huo utendaji wake umekuwa ni mbovu na hivyo kusababisha wafanyabiashara wakubwa ndani na nje ya nchi kuancha kutumia basndari hiyo na hivyo kutumia  bandari ya Mombasa.
BANDARI YA DAR ES SALAAM.
 Dkt . mwakyembe amesema bandari hiyo imekithiri ubabaishaji,wizi,pamoja na gharama za kutolea mizigo  na ushawishaji kutoongezeka hali inayochangia wafanyabishara wengi kutotumia bandari hiyo.

Kitendo cha kuwasimamishwa kazi baadhi ya watendaji katika mamlaka hiyo kimechangia kurudisha utendaji kazi na imani kwa wafanyabishara wakubwa ndani na nje nchi ambapo baadhi yao tayari wameanza kujitokeza kwa ajili ya kufanya kazi na mamlaka hiyo.

No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...