Monday, October 22, 2012

JE NI NANI KALA NYAMA YA MTU - MWALIMU JK. NYERERE ?





Katika siku za hivi karibuni kumekuwepo na mjumuiko makundi mbalimbali  mengi yakionekana  kutumia  dhana ya dini kufikisha hisia ama matakwa binafsi  kwa jamii, pasipo kufuata taratibu  ama sheria za nchi

Pamoja na uwepo wa usajili halali wa vikundi hivyo ,bado njia ama taratibu ambazo zimekuwa zikifuatwa  na vikundi hivyo zimeonyesha madhara makubwa ,ndani ya nchi  hali inayosababisha kutoweka kwa amani.

Shughuli za kiuchumi zimekuwa zikilazimika kusimama  kwa muda  kutokana na ghasia ambazo zimekuwa zikisababishwa  vikundi hivyo pale vinapotakaka  kuzuiliwa kufikisha hisia zao kwa jamii.

Wengi tumeshuhudia ghasia mauwaji yaliyotokea katika miji ya mombosa nchini Kenya kufuata kukamatwa kwa kiongozi wa kundi la MRC linalotaka kujitenga kwa eneo la pwani na jamhuri ya Kenya 

Kutoweka kwa sheikh Farid Had  kiongozi wa kundi la Uamsho visiwani Zanzibari, kukamatwa kwa sheikh ponda issa pondo katika jiji la Dar es salaam,ni miongoni mwa  sababu nyingine zilizosababisa vurugu ama ghasia na kupelekea kusimama kwa shughuli za kiuchumi  kuharibiwa kwa mali  

Pamoja na hayo, Uhuru wa kujielezea ni jambo muhimu kwa kila mmoja  pasipo kuingilia uhuru wa mwenzake, kiungo hiki kinaweza  kudumu pale tu kitakapokuwa hakihusianishwi na suala la dini.

Katika nchi mbalimbali duniani madhara  mengi yameonekana  pale dhana ya udini inapotumika Kufikisha fikra ama mitazamo Fulani kwajamii, kumekuwepo na hali ya kutosikilizana huku kila mmoja akiona imani yake ni sawa kuliko ya mwenzake

Mfano hai wa nchi hizo ni pamoja na Misri ,Nigeria  ,Sudan Libya Iraq Pakistan na nyinginezo ambapo katika mataifa hayo utawala halali umekuwa katika wakati mgumu katika kuziba nyufa mdani ya taifa

Madhara ya kutumia dini kama kigezo cha kufikisha fikra ama hisia binafsi tayari yameonekana nchini nigeria ,boko haram kundi lilianza kaskazini mwa nigeria mnamo miaka ya 2001 likiwa  kama kundi dogo lililokuwa likipinga mitazamo na elimu za kimagharibi 

Katika harakati zake ,kundi hili sasa limekuwa ligonga vichwa vya wengi kutokana kukataa utawala wa sheria zilizotungwa , na hata mambo muhimu yanayohusu utandawazi

Kikubwa ambacho kimekuwa kikipiganiwa na kundi hilo ni kudai utawala wa kidini wa sharia ili hali nchi ya Nigeria ikongozwa pasipo kufuata misingi kidini  ,hali hiyo imesababisha  kutokuwepo kwa maelewano baina ya serikali na kundi hilo  hivyo kusababisha machafuko makubwa ndani ya nchi hiyo kila kunapokucha.

Katika harakati ya kudai utawala huo kundi hilo sasa linaendesha mashamulizi dhidi ya serekali ,taasisi binafsi  ,waumini wa dini ya kristo lakini pia kwa waislamu wasio kubali misingi ya kundi hilo.

Tangu kuanza kwa harakati hizo maelfu ya ya watu wameangamizwa 

Tayari tabia na namna ya makundi hayo yanavyofanya kazi yanafanana na baadhi ya makundi nchini Tanzania ambayo yanajipambanua kwa misingi ya kidini lakini nyuma yake ni makundi hatari kwa umoja na mshikamano wa taifa letu.

No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...