Friday, October 12, 2012



GHASIA KUBWA ZIMEIBUKA MBAGALA BAADA YA MTOTO MMOJA KUKOJOLEA KURAAN

POLISI WA KUTULIZA GHASIA  WAKITANDA ENEO LA MBAGALA KUZUIA KUENDELEA KWA VURUGU
Ghasia kubwa zimeeibuka katika eneo la mbagala kizuiani jijini Dar  es laam baada ya  mototo mmoja anaedaiwa kuwa mkristo  kukujolea  kitabu tukufu cha kuruani wakati akitaniana na mwenzie.

Kufuatia kitendo  hicho  kumezuka kumezuka vurugu baada ya wafuasi wa dini ya kiislamu kuvamia kituo cha polisi wakitaka kuadhibiwa kwa motto huyo anayedaiwa kuwa na umri wa miaka 14.
BAADHI YA WANAFUNZI MARA BAADA YA KUFYETULIWA KWA MAVBOMU YA MACHOZI.

Polisi katika kituo cha mbaghala wamesimama kidete  kumkinga kijana huyo ndipo sasa  baadhi ya waumini walipoamua kujichukulia sheria mkononi  kwa kuanza kuvunja vioo vya  magari yaliyokuwemo kituoni hapo yakiwemo ya pilisi

MAMIA YA WAISLAM WAKIWA KATIKA KITUO CHA POLISI MBAGALA LEO JIJINI  DAR ES SALAAM
Baadhi yao walianza kuweka magogo  na matofali katika barabara  zinazozunguka kituo hicho  ili kuzuia magari kuingia    na pia  kutoka lakini baada ya muda polisi wa kutuliza ghasia  walifika na kuwataka kutawanyika.
Baada ya kukaidi amri hiyo polisi wamelazimika kutumia mabomu ya machozi ,na kuwakamata baadhi yao  na kuwapeleka kituo cha polisi Chang’ombe.

Makundi mengine ya  waislamu wameondoka kituoni hapo na kuanza kwenda kuchochea vurugu  kwa kuchoma baadhi ya makanisa  eneo la Chamanzi  kwa madai kuwa wanalipiza kisasi.

Hadi kufikia sasa mototo huyo anasshikiliwa na polisi kwa lengo la kufunguliwa mashtaka kutokana na kitendo hicho

No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...