Wednesday, September 5, 2012


           HALI YA  WANANCHI WA SYRIA INATISHA ASEMA LAKHDAR BRAHIMI
Lakhdar Brahimi mpatanishi wa mzozo wa syria
 Mpatanishi wa kimataifa wa mzozo wa Syria,Lakhdar Brahimi ametoa picha ya kutisha ya hali nchini Syria,akiitaja idadi ya wahanga ni ya "kushtusha" na "maangamizi yasio na kifani "yaliyosababishwa na vita nchini humo 

Katika wakati ambapo mzozo wa Syria unaingia katika mwezi wa 18,bila ya kuwepo matumaini ya kuupatia ufumbuzi,matumizi ya nguvu yanazidi makali-pekee hii leo watu wasiopungua 20 wameuwawa jeshi la serikali lilipouhujumu mji wa Aleppo,walikopiga kambi waasi,zaidi ya mwezi mmoja uliopita.

Katika hotuba yake ya kwanza mbele ya hadhara kuu ya Umoja wa mataifa mjini New-York,tangu alipoanza rasmi shughuli zake kama mpatanishi wa mzozo wa Syria,Lakhdar Brahimi amezungumzia ziara anazopanga kufanya hivi karibuni mijini Damascus na Cairo.-

Anahisi ni muhimu kupata uungaji mkono wa jumuia ya kimataifa ambayo haina msimamo mmoja linapohusika suala la namna ya kuupatia ufumbuzi mzozo wa Syria;warusi,wachina na wairan-washirika wa utawala wa Bashar al Assad wakipinga mpango wowote wa kuingiliwa mzozo huo na mataifa ya kigeni ,huku nchi za magharibi na washirika wao wa kiarabu wakiwaunga mkono waasi.

"Idadi ya wahanga inamfanya mtu aduwae,hali inazidi kuwa mbaya" ameonya mwanadiplomasia huyo aliyeshika nafasi iliyoachwa na Kofi Annan na kufafanua umuhimu wa ushirikiano wa jumuia ya kimataifa.

Bwana Lkhdar Brahimi ameongeza kusema:"Mustakbal wa Syria utaamuliwa na wananchi wake wenyewe na sio na wengine.Uungaji mkonmo wa jumuia ya kimataifa ni jambo la lazima na linalohitajika haraka.Uungaji mkono huo utaleta tija tu ikiwa wote watakuwa na msimamo mmoja."
Ban Ki-Moonkatibu  mkuu wa Umoja wa mataifa
 Nae katibu mkuu wa Umoja wa mataifa Ban Ki-Moon,akihutubia pia mbele ya hadhara kuu ya Umoja wa mataifa mjini New York,amezikosoa nchi zinazozipatia silaha pande zinazohasimiana nchini Syria na kutoa wito wa kuwepo mshikamano wa jumuia ya kimataifa ili kuwapatia huduma za kiutu wakimbizi wa Syria ndani na nje ya nchi hiyo.

Urusi na Iran zinatuhumiwa kuupatia silaha utawala wa Bashar al Assad huku Saud Arabia na Qatar zikitajwa kuwapatia silaha waasi.

No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...