Tuesday, September 4, 2012


 
DOS SANTOS  KUONDOZA KIPINDI KINGINE CHA MIAKA MITANO ANGOLA

Hatimae chama tawala nchini Angola cha MPLA kinachongozwa na  rais Jose eduardo dos Santos kimetangazwa rasmi kuwa kimeshinda uchaguzi uliofanyika  nchini humo siku ya jumaa iliyopita.

Haijulikani sababu hasa lakini Vyombo vya habari vya serikali vilitangaza taarifa hiyo hata kabla ya matokeo ya mwisho kutolewa.

 Hatua hiyo inampa rais  dos Santos hatamu ya uongozi wa miaka mingine  mitano zaidi kubeba majukumu ya uongozi huo wa ngazi ya juu kabisa katika nchi.

 Kutokana na mabadiliko ya katiba ya mwaka 2010 ni kwamba kiongozi wa chama kilichopata kura nyingi zaidi ndie anayepaswa kutawazwa kuwa rais na kiongozi mkuu wa mkuu washughuli za  serikali. 

Kwa mujibu Taarifailiyotolewa na  Tume ya Uchaguzi na kutangazwa katika mji mkuu Luanda imesema kuwa  asilimia 75 ya wapiga kura wamekichagua chama  cha MPLA kuendelea kuwa chama tawala nchini humo



                             
Chama kikubwa kabisa cha upinzani, UNITA, kilipata asilimia 18 ya kura ambapo  Msemaji wa upinzani na waangalizi huru wa uchaguzi huo awali wamelalamikia tume ya uchaguzi kwamba hajaridhishwa kutokana na kuwepo  kasoro katika zoezi la uchaguzi huo.


Huu ni uchaguzi wa tatu nchini Angola tangu ipate uhuru wake kutoka kwa Wareno mwaka 1975. Uchaguzi wa mwisho ulifanyika mwaka 2008.

No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...