Tuesday, August 28, 2012


       MACHAFUKO YAENDELEA KATIKA MJI WA MOMBASA NCHINI KENYA

Machafuko yameukumba mji wa Mombasa, baada ya vijana wenye hasira kushambulia maeneo mbalimbali katika mji huo

Polisi wa Kenya walivamia maandamano ya vijana hao waliokuwa wanalalamikia kuuawa mhadhiri mmoja wa Kiislamu Sheikh Aboud Rogo. Marekani inadai kuwa Sheikh Rogo alikuwa na uhusiano na kundi la ash Shabab la Somalia.

Jana Sheikh Rogo alifyatuliwa risasi na watu wasiojulikana katika viunga vya eneo la Malindi mjini Mombasa katika barabara kuu ya Bumburi na aliuawa ndani ya gari yake wakati alipokuwa anampeleka mke wake hospitalini.
Kenyan security forces patrol the streets during demonstrations following the shooting and killing of Aboud Rogo Mohammed, in Kenya's coastal city of Mombasa, August 27, 2012. REUTERS/Joseph Okanga
Gari la Sheikh Aboud Rogo lilivyoshambuliwa
 Awali polisi ya nchi hiyo ilikuwa ilitangaza kuwa, Aboud Rogo aliuawa kwa tuhuma za kuliunga mkono na kulisaidia kundi la ash Shabab la Somalia.

Hata hivyo Waislamu wa mjini Mombasa wamepinga tuhuma hizo dhidi ya Rogo na kusema kwamba marehemu hakuwa na mahusiano na kundi hilo. 

Sheikh Aboud Rogo enzi ya uhai wake.
 Waislamu hao wameongeza kuwa, suala lililopelekea kuuliwa Sheikh Aboud Rogo, ni msimamo wake wa kupinga muswada wa sheria ya ugaidi ambao umekuwa ukipingwa na Waislamu wa Kenya wanaoamini kuwa, sheria hiyo ina lengo la kuwakandamiza.
.

No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...