Friday, June 1, 2012

Bodi ya upatanishi ya Jumuya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika, SADC, imesema itaandaa mkutano maalum utakaowakutanisha kiongozi wa mpito wa Madascar, Andry Rajoelina, na rais wa zamani wa kisiwa hicho, Marc Ravalomanana.

Viongozi wa mataifa 15 wanachama wa SADC wameamua kuwakutanisha mahasimu hao wawili ikiwa kama jitihada ya kusuluhisha mgogoro wa kisiasa unaokikabili kisiwa hicho kwa takribani miaka mitatu sasa.

 Katika kauli ya pamoja iliyotolewa katika mkutano wa kilele wa jumuiya hiyo uliyofanyika katika mji mkuu wa Angola, Luanda, inaeleza kuwa shabaha kuu ni kuandaa muongozo wa kumaliza mgogoro na kuweka mazingira mazuri ya kufanyika uchaguzi huru na wa haki.

Mgogoro katika kisiwa hicho kilicho katika Bahari ya Indi ulizuka Machi 2009, pale ambapo Rajoelina alimuondoma madarakani Ravalomanana kwa kusiadiwa na jeshi la taifa hilo.


No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...