Mahakama ya
Hakimu Mkazi Arusha imeahirisha shauri la kesi inayomkabili Mbunge wa Jimbo la
Arusha Mjini, Mh Godbless Lema (CHADEMA), kwa tuhuma za kuchochea vurugu katika
Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) hadi Octoba 1, 2013 ambapo mashahidi wa
upande wa mashitaka wataanza kutoa ushahidi wao kwa siku mbili mfululizo.
mashahidi wa kesi ya uchochezi inayomuhusu mbunge wa jimbo la Arusha Godbless Lema ,Nyuma ni mshauri wa wanafunzi (Dean of student) akizungumza na Ispekta Bernad. |
Hakimu Msofe aliwataka mashahidi wote kama walivyohuduria leo kufika Mahakamani hapo siku ya Jumanne na Jumatano ya Oktoba 1 na 2 kwa ajili ya kuanza kutoa ushahidi wao, zoezi ambalo lilipangwa kuanza leo kama kuningekuwa na udhuru wa kuahirisha shauri hilo.
Mashahidi wa upande wa mashitaka .anaeongea na simu ni Makamu Mkuu wa Chuo cha IAA, Bw Faraj Kasidi na anaemtazama ni Jane Chibuga. |
Wengine ni Inspekta wa Polisi Bernad Nyambalya, Makamu Mkuu wa Chuo cha IAA Bw Faraj Kasidi na Jane Chibuga.
Awali Wakili Kimomongoro anayemwakilisha Lema wakisaidiana na Wakili Humrefy Mtui aliwasilisha ombi la kuiomba Mahakama iahirishe shauri hilo hadi tarehe nyingine kwa kile alichoeleza kuwa ni kutokana na Mh Lema kuwa katika hali ya kuumwa na kwamba ni jana tu aliruhusiwa kutoka hospitali ya AICC alikokuwa amelazwa tangia Agosti 14 akiendelea kutumikia siku 10 alizopewa na daktari za mapumziko ya kitandani.
Inspekta Bernad Nyambalya akisalimiana na Mawakili wa Mh Lema mara baada ya kesi hiyo kuahirishwa. Kulia kabisa ni Mwanasheria Glory Kaaya. Picha zote na Seria Jr. |
No comments:
Post a Comment