Wednesday, August 21, 2013

FILAMU MPYA YA “TABIA” YAZINDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM


PIX 1

Katibu wa bodi ya filamu nchini Bi  Joyce  FISOO akionyesha bango la filamu mpya "TABIA'' mara baada ya kuzindua filamu hiyo jijini hapa.

http://www.fullshangweblog.com/wp-content/uploads/2013/08/PIX-31.jpg 

Baadhi ya wasanii maarufu wakisikiliza hotuba ,wakati wa hafla hiyo .

PIX 5 

Baadhi ya wasanii na wageni waalikwa wakiangalia filamu hiyo mara baada ya kuzinguliwa na katibu mtendaji wa bodi ya filamu nchini  bi JOYCE FISSOO 

Uzinduzi wa filamu hiyo ulifanyika hivi karibuni katika Ukumbi wa Hoteli ya May Fair Plaza uliopo Mikocheni jijini Dar es Salaam.

Katika unzinduzi wa filamu hiyo, Bi Fissoo amebainisha kuwa filamu ya TABIA imekaguliwa na Bodi ya Filamu na kupewa daraja 13 yaani filamu hii inaruhusiwa kutazamwa na watu kuanzia miaka 13 na kuendelea

“Ni filamu inayoweza kuonwa na wanajamii wengi kwani imejikita katika kuelimisha kuanzia kwa watoto wetu”. Alisema Bi. Fissoo.

Bi Fissoo alisema kuwa hapa nchini ni filamu chache zinazojikita katika kundi hilo ambazo zinawasilishwa Bodi ukilinganisha na zile zinazolenga umri wa miaka 18 na kuendelea.

Aidha, Bi Joyce ameipongeza Kampuni ya Harmony kwa kuthubutu kwao na ana imani kuwa Kampuni hiyo itaendelea kuzalisha filamu bora zenye weledi, maadili na zinazoweza kuingia katika soko la ushindani.

Filamu ya TABIA ni filamu mpya iliyoandaliwa na kutengenezwa na Kampuni ya Harmony ambayo ni moja ya kampuni iliyowekea kazi zake stamp za TRA ambazo lengo lake ni kuondokana na wizi wa kazi za wasanii hapa nchini.

No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...