Thursday, December 13, 2012

RAIS KIKWETE: WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUWA NA DIGRII

Rais Jakaya Mrisho Kikwete amesema ifikapo mwaka 2015 hakutakuwa na uhaba wa walimu nchini humo na kwamba kuanzia mwaka 2020 shule za msingi zitaanza kufundishwa na walimu wenye elimu ya shahada, kutokana na idadi kubwa ya wahitimu wa fani hiyo watakaokuwa kwenye soko la ajira. 

Akizungumza kwenye kongamano linalohusu masuala ya uchumi na maendeleo lililoandaliwa na Kigoda cha Mwalimu Nyerere kwa kushirikiana na Kitivo cha Uchumi cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Rais Kikwete amesema , katika sekta ya elimu licha ya kuwa na changamoto kadhaa, lakini serikali imepiga hatua kubwa ya maendeleo kutokana na kuongezeka kwa idadi ya wanafunzi wanaoandikishwa kwenye darasa la kwanza, wanafunzi wa sekondari na vyuo vikuu na vile vya ufundi. 

Hata hivyo Rais Kikwete amekiri kwamba Tanzania inakabiliwa na upungufu wa walimu wa masomo ya sayansi, na kwamba jambo hilo linapaswa kutafutiwa suluhisho.

      

No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...