Amiri
Jeshi mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania,Mh. Dkt. Jakaya
Mrisho Kikwete akiwasili katika Uwanja wa Uhuri akiwa kwenye gari maalum la
Kijeshi na Sambamba na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama,Jenerali Davis
Mwamunyange walipokuwa wakioa salamu kwa wananchi na wageni mbali mbali
waliofika Uwanjani hapo kwa ajili ya maadhimisho ya miaka 51 Uhuru wa Tanzania
Bara.Kauli Mbiu ya Maadhimisho ya Mwaka huu ni “Uwajibikaji, Uadilifu na
Uzalendo ni nguzo ya Maendeleo ya Taifa letu”.
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania,Mh. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akikagua gwaride la vikosi vya Ulinzi
na usalaama katika maadhimisho Miaka 51 ya Uhuru wa Tanzania Bara,leo katika
Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam.
Amiri
Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mh. Dkt. Jakaya Mrisho
Kikwete pamoja na viongozi wengine wa Serikali wakipokea salamu za heshima
kutoka kwa Vikosi mbali mbali vya Ulinzi la Usalama wakati wa maadhimisho ya
miaka 51 ya uhuru wa Tanzania Bara yaliyofanyika leo kwenye uwanja wa Uhuru
jijini Dar es salaam.
Kikosi
cha Brass Band cha majeshi ya Ulinzi na usalama kikitumbuiza katika maadhimisho
hayo.
Vijana
wa chipukizi wakionyesha michezo na ujumbe mbalimbali wakati wa maadhimisho
hayo.
Vikosi
vya Ulinzi na Usalama vikiwa vimejipanga tayari kwa gwaride la utii na heshima
mbele ya Amiri jeshi Mkuu na Rais Jamhuri ya muungano ya Tanzania,Mh. Dkt.
Jakaya Mrisho Kikwete
|
No comments:
Post a Comment