Nyumba
iliyobomoka kutokana na mvua iliyoambatana na upepo mkali.
|
ZAIDI ya familia ya 300 katika Kijiji cha Migoli,
Iringa Vijijini, hazina mahali pa kuishi kufuatia nyumba zao kubomoka na
nyingine kuezuliwa kwa upepo ulioambatana na mvua kubwa.
Mvua
hiyo iliyonyesha juzi, ilianza saa 8:00 mchana ikiambatana na upepo mkali
uliosambaratisha nyumba 57.
Nyumba
38 miongoni mwa hizo, zimezuliwa na nyingine 19 zimebomoka.
Diwani wa kata hiyo, Husein Kiswili. alilithibitisha habari kuhusu tukio hilo na kwamba uharibifu huo umehusisha pia miundombinu ya umeme na barabara katika eneo hilo.
““Hali
ni mbaya sana, watu hawana makazi kwa sababu nyumba nyingine zimeanguka, umeme
umekatika kwa sababu nguzo zimeangushwa,” alisema Kiswili.
Alisema
mbali na nyumba za wananchi pia baadhi ya vyumba vya madarasa ya
shule ya msingi, vimeezuliwa na hivyo kusababisha wanafunzi kukosa masomo.
Diwani
huyo alisema wakazi wa kijiji hicho kwa sasa wanahitaji msaada wa haraka wa
kibinadamu.
Mbunge wa Isimani, William Lukuvi, alisema ameagiza timu ya maafa ifanye tathmini kuhusu hasara iliyowakumba wananchi hao, ili aifanyie kazi.
Lukuvi
pia aliahidi kutoa mabati kwa ajili ya kuezeka vyumba vya madarasa
vilivyoezuliwa na upepo huo.
Kwa
upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dk Christine Ishengoma, alitoa kilo
750 zachakula ili kusaidiwa waathirika wa tukio hilo.
Pia
aliwataka wananchi kuwa wavuliivu na kusaidiana katika kipindi hiki kigumu.
Dk Ishengoma alisema Serikali inafanya tathimini ili kujua kiwango cha
hasara iliyopatikana kutokana na mvua hiyo.
No comments:
Post a Comment