Friday, October 19, 2012

HALI YA TAHARUKI  YAENDELEA KUTANDA KATIKA VIUNGA VYA JIJI LA DAR ES SALAAM.


Taarifa kutoka   katika viunga vya jiji  la dar es salaam zikaneleza , hali ya taharuki imeendelea kutanda punde tu mara baada ya kumalizika kwa swala ya ijumaa.

Vurugu kubwa zimetokea mchana huu katika maeneo yanayozunguka soko kuu la Kariakoo na kusababisha hofu kubwa  huku Polisi wakilazimika kutumia mabomu ya machozi na kutawanya mikusanyiko ya watu waliokuwa wamejiandaa kuandaamana
ASKARI WA POLISI WAKIMHIMIZA MMOJA WA  WAUMINI WA DINI YA KIISLAMU ALIYEKAMATWA KATIKA VIUNGA VYA IKULU JIJINI DAR ES SALAAM
 Taarifa zaidi zinasema kuwa katika eneo la Magomeni  msikiti wa Kichangani ,baadhi ya waumini wa dini ya kiislamu,wanadaiwa kumshambulia sheikh mmoja kufuatia sheikh huyo kuwazuia kuandamana. 
 

Hata hivyo taarifa kutoka eneo la tukio zinasema kuwa, waumini hao wameweza kutawanywa lakin  hali bado tete huku magari ya jeshi la Polisi yakielekea katika maeneo ya Kinondoni ambapo kunadaiwa kuwa hali si shwari na vurugu kama hizo zinaendelea.


Maduka yote katika maeneo hayo yamefungwa na shughuli mbalimbali zimesimama pamoja na Ofisi mbalimbali zimefungwa kutokana na hofu kubwa iliyotanda.

Baadhi ya waumini wa dini ya kiislamu wamekuwa wakiandamana kushinikiza kuachiwa huru kwa kiongozi wa jumuiya ya waislamu sheikh Ponda Issa Ponda wakifuata waraka uliotolewa na jumuiya ya waislamu
Picture
HALI ILIYVYOKUWA KALEO KATIKA JIJI LA DAR ES SALAAAM





Picture na wavuti.com

No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...