Tuesday, October 2, 2012



AJALI YA MBALIZI YAGHARIMU MAISHA YA WATU WENGI

Miili ya watu  tisa imeeungua vibaya na kutawanyika baada ya lori lililokuwa na mafuta linalosadikiwa ni mali ya kampuni la LAKE OIL lenye namba za usajili T 814 BTC lililokuwa na tela ambalo namba zake ahazitambulika mara moja kufuatia kuungua vibaya.

Habari zaidi zinaeleza kuwa ajali hiyo imehusisha magari matatu, Lori lililokuwa na namba za usajili T 299 BCE lililokuwa likishuka taratibu mteremko wa Mbalizi ,Hiace T 887 AHT inayofanya safari zake Mbalizi na Mwanjelwa na Gari Ford Double Cabin linalosadikiwa kumilikiwa na Mbunge wa Viti Maalum kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi, Mary Mwanjelwa ambalo namba zake hazikupatikana mara moja kutokana na kuungua .
Sadiki Nurdin ambaye ni utingo wa Lori lenye namba T 299 BCE amemwambia mwandishi wa habari hii kwamba lori lilikuwa na mafuta likiwa nyuma yao aliliona likija kwa mwendo kasi  hivyo alimshtua dereva wake na hivyo kulikwepa.

Mabaki ya lori lililokuwa na mafu

Utingo huyo amesema  walipolikwepa lilianza  kula ubavu wa gari lao na hatimaye lilikwenda na kukutana uso kwa uso na Hiace pamoja na gari linalosadikiwa ni la Mbunge wa Viti Maalum CCM na kusababisha maafa hayo.

Tarifa ambazo hazikuthibitishwa zimeeleza kuwa waliokufa ni 9, wawili kutoka kwenye Lori ambalo limelipuka na kusababisha maafa hayo, watu 6 kutoka kwenye basi la abiria aina ya HIACE, mpanda baiskeli, na mwendesha bodaboda.

Umati wa raia ukishuhudia ajali hiyo ,yaliyotapakaa ni mafuta yaliyokuwa yamebebwa kwenye matank ya lori lililoteketea kwa moto

Idadi ya majeruhi  bado ,hajipata bado licha ya kwamba wamefikishwa katika hospitali ya Ifisi Mbeya Vijijini.
Zoezi la uokoaji kwa mara ya kwanza limefanywa chini ,Koplo Mathias Joachim wa  Kikosi cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania 44 KJ Mbalizi Mbeya.

Mkuu wa mkoa wa Mbeya ABBAS KANDORO akiambatana na viongozi mbalimbali kushuhudia tukio hilo.

Ajali hii inakuja ikiwa ni siku chache tu zimepita tangu kumalizika kwa wiki ya nenda kwa usalama babarani ambayo pamoja na mambo mengine elimu pamoja na msisitizo kuusu sheria na kanuni za barabarani zimesisitizwa 



Katika hatua nyingine basi la abiria la kampuni ya Dar Express limepata ajali ya kuungua na kuteketea kwa moto , katika eneo la Segera kwenye njia panda ya Dar es Salaam-Arusha-Tanga.



Basi la kampuni ya Dar Express likiteketea kwa moto katia eneo la Segera mkoani tanga

 

1 comment:

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...