Thursday, November 15, 2012

CHINA.

MABADILIKO YA UONGOZI CHINA : XI JINPING RAIS MPYA
XI JINPING RAIS MPYA WA CHINA

Chama  tawala  cha  kikomunist  nchini  China  leo kimetangaza  baraza  jipya  la  uongozi  litakalokuwa  na wajumbe  saba  wakiongozwa  na  Xi Jinping, ambaye ataongoza nchi  hiyo  yenye  uchumi  wa  pili  kwa  ukubwa duniani  kwa  kipindi cha  muongo  mmoja  ujao.

Xi ambaye  anachukua  nafasi  ya  katibu  mkuu  wa chama  ambaye  amemaliza  muda  wake rais Hu Jintao, amesema  kuwa  anataka  kupambana  na  rushwa  na kujenga  maisha  bora  kwa  raia bilioni 1.3  wa  nchi hiyo.
ALIYEKUWA RAIS WA CHINA HU JINTAO.


Katika  hotuba  yake  ya  kwanza  ameahidi  kutimiza wajibu  waliopewa  na  chama  hicho.


Xi mwenye  umri  wa  miaka  59, atathibitishwa  kuwa kiongozi  wa  nchi  hiyo  na  bunge  mwezi  Machi mwakani.


No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...