Friday, October 19, 2012



MWANAFUNZI AUWAWA KWA RADI WAKATI AKIJISOMEA NA WENZAKE.

Mwanafunzi  wa kidato cha kwanza, Shue ya Sekondari Chamriho iliyoko Wilayani Bunda, Mkoani Mara amefariki dunia kwa kupigwa na radi na wenzake watatu wamenusurika baada ya nyumba waliyokuwemo kuteketea kwa moto.

Tukio hilo  limetokea katika Kijiji cha Nyang’aranga, kata ya Mugeta  Wilayani  Bunda majira ya saa tatu usiku wakati marehemu na wenzake wakijisomea ndani ya nyumba hiyo na radi kuleta maafa na majonzi ya kupotelewa mwanafunzi mwenzao. 

Afisa mtendaji wa kijiji hicho  Fikiri Magunila  amemtaja  mwanafunzi aliyepigwa na radi kuwa ni Karosi Joramu aliyekuwa akisoma  kidato cha kwanza shule ya secondary chamriho.
Bwana Magunila amesema kuwa tukio hilo la radi lilisababisha nyumba hiyo kuwaka moto na kuteketea huku wanafunzi watatu wakiyanusuru maisha yao. 

Kumekuwepo na matukio ya radi katika kijiji hicho ambapo miaka ya hivi karibuni radi iliua watu wawili.

Soure-wotepamoja.com

No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...