Tuesday, June 26, 2012


              
               SERIKALI YA UTURUKI YAENDELEA KUHITUHUMU NCHI YA SYRIA 

Uturuki imewasilisha rasmi malalamiko yake mbele ya Umoja wa Mataifa UN ikidai kutunguliwa kwa ndege yake kulikofanywa na Syria ni kitisho juu ya amani katika eneo hilo na lazima juhudi zifanyike kudhibiti vitendo hivyo.

Moja ya ndege za Uturuki zilizoangushwa na serikali ya Syria

 

Malalamiko hayo ya Uturuki yanawasilishwa kipindi hiki ambacho Wanachama wa Jumuiya ya Kujihami ya Nchi za Magharibi NATO wanakutana jumanne kujadili hatua ya kutunguliwa kwa ndege hiyo.

Viongozi wa Jumuiya ya kujihami ya nchi za Magharibi NATO

Katika hatua nyingine Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa UN Ban Ki Moon amesema wakati umefika kwa Baraza la Usalama la kufanya kila linalowezekana ili kuwalinda wananchi.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa UN Ban Ki Moon

Syria imeendelea kukabiliwa na shinikizo linalomtaka Rais Bashar Al Assad kuhakikisha anafanya kila liwezekanalo kuruhusu demokrasia kuchukua mkondo wake au akae kando.


Rais wa Syria    Bashal Al Assad


No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...