Monday, October 8, 2012



HUGO CHAVES RAFAEL FRIAS KIONGOZI WA VENEZUELA  MWENYE MSIMAMO USIOTEREREKA.
HUGO CHAVEZ-RAIS WA VENEZUELA.
Ikiwa tunashuhudia  safari nyingine ya kuelekea miaka sita kwa kiongozi huyu wa Venezuela nayedaiwa kuwa misimamo isiyoterereka  nimeona ni vema tukamtazamia je alikotoka ni wapi  na anakoelekea

Hugo Rafael Chavez Frias alizaliwa Julai 28, 1954. Alishika madaraka ya kuiongoza Venezuela mwaka 1999.

Kufuatia itikadi yake ya kisiasa ya Kibolivarian na "Usoshalisti wa karne ya 21", amelenga katika kutekeleza mageuzi ya usoshalisti katika nchi kama sehemu ya mradi wa kijamii inayojulikana kama Mapinduzi ya Wabolivia, ambayo yameshuhudia utekelezaji mpya wa katiba, demokrasia shirikishi na kutaifisha viwanda kadhaa muhimu.

Alizaliwa Sabaneta, Barinas, akawa afisa kazi jeshini, na baada ya kutoridhika na mfumo wa siasa za Venezuela ambao aliuona kama wa rushwa na sio wakidemokrasia, alianzisha Vuguvugu la siri la Mapinduzi ya Kibolivarian-200 (MBR-200) katika miaka ya 1980 ili kuipindua serikali.

Add caption

Baada ya tukio la kidemokrasia serikali ya Rais Carlos Perez Andres aliamuru ukandamizaji mkali wa maandamano dhidi ya kupunguzwa matumizi, Chávez aliongoza MBR-200 katika mapinduzi yaliyoshindwa dhidi ya serikali mwaka 1992, ambapo aliishia kufungwa jela.

Alipotoka gerezani baada ya miaka miwili, alianzisha chama cha siasa, Fifth Republic Movement, na alichaguliwa kuwa rais wa Venezuela mwaka 1998. Hatimaye alipendekeza katiba mpya ambayo iliongeza haki kwa makundi yaliyotengwa na ilibadilisha utaratibu wa serikali ya Venezuela, na alichaguliwa tena mwaka 2000.
 

Wakati wa muhula wake wa pili wa urais, alianzisha mfumo wa Misheni ya Kibolivarian, Halmashauri za Kijamii na vyama vya ushirika vinavyosimamiwa na wafanyakazi, wakati pia alitaifisha viwanda mbalimbali muhimu kwa maslahi ya taifa.

Wapinzani wakati huohuo, walionesha hofu kwamba alikuwa akiumomonyoa uwakilishi wa kidemokrasia na kujiongezea mamlaka, walijaribu kumwondoa madarakani kwa njia zote kupitia mapinduzi ya kijeshi yaliyoshindwa mwaka 2002 na kura ya maoni ya kukumbukwa mwaka 2003.
 

Alichaguliwa tena mwaka 2006, kufuatia kuanzisha chama kipya cha siasa, United Socialist Party of Venezuela (PSUV), mwaka 2007. anajulikana kama mkosoaji wa ubepari na hasa uliberali wa kisasa, Chávez amekuwa mpinzani maarufu wa sera za kigeni za Marekani.

 Akifungamana mwenyewe na serikali ya ujamaa ya Fidel na kisha Raul Castrol ya Cuba, ya Evo Morales wa Bolivia, na ya Rafael Correa wa Ecuador. Urais wake unaonekana kama sehemu ya “mrengo wa kushoto” ukiisafisha Amerika ya Kusini.

Amekuwa anaunga mkono ushirikiano wa Amerika Kusini na Caribbean na alikuwa mtu muhimu katika kuanzisha ushirikiano wa kanda nzima; Umoja wa Mataifa ya Amerika Kusini, Muungano wa Wabolivia kwa ajili ya Waamerika, Benki Kuu ya Kusini, na mtandao wa televisheni wa kikanda, TeleSur. Ushawishi wake wa kisiasa katika Amerika ya Kusini ulimfanya jarida la Time kumuweka katika orodha ya watu 100 wenye ushawishi mkubwa zaidi duniani katika miaka ya 2005 na 2006.

Maisha ya awali: 1954-1970

Hugo Chávez alizaliwa katika nyumba ya upande wa bibi yake mzaa baba, Rosa Inéz Chávez (aliyefariki 1982), kwenye kibanda cha matope cha vyumba-vitatu iliyoko kijiji cha Sabeneta, Jimbo la Barinas.

Wazazi wake, Hugo de los Reyes Chavez na Elena Frias de Chavez, walikuwa walimu – wa tabaka la chini kati - waliokuwa wakiishi katika kijiji kidogo cha Los Rastrojos, na kabla ya kuzaliwa Hugo walikuwa tayari na mtoto mmoja, Adan Chavez, na baada ya Hugo walipata watoto wengine watano zaidi, ingawa mmoja wao, Enzo, alikufa kwenye umri wa miezi sita. Familia ya Chávez ilikuwa ya mchanganyiko wa asili ya Amerindia, Afro-Venezuela, na Kihispania. 
 

Waliishi katika umaskini, hasa Hugo na ndugu yake Adan waliishi na bibi yao Rosa, ambaye baadae Hugo alimuelezea kuwa "binadamu safi... mwenye upendo, mwema." Alikuwa mcha Mungu, Mkatoliki, na Hugo mwenyewe alilelewa katika imani, kijana wa madhabahu ya kanisa la mtaa.

Chávez alijua kwamba yeye na ndugu yake "tulikuwa maskini sana lakini watoto wenye furaha sana", na kwamba "Kwa upande wa (Rosa) bibi, nilijua unyenyekevu, umaskini, maumivu, na wakati mwingine kutokuwa na kitu chochote cha kula. Nikaona ukosefu wa haki katika dunia hii."


Mafunzo ya Kijeshi: 1971–1975

Akiwa na miaka kumi na saba, aliamua kwenda kusoma katika Chuo cha Sayansi ya Jeshi cha Venezuela mjini Caracas, baadaye alisema kwamba "nilijihisi kama samaki katika maji. Kama nimegundua sehemu ya kiini cha maisha, wito wangu wa kweli."

Katika Chuo, alikuwa mwanachama wa daraja la kwanza aliyefuata mitaala ya marekebisho inayojulikana kama Mpango wa Andres Bello

 Mpango huu uliwekwa na kundi la maendeleo, maafisa wa kijeshi walioamini mabadiliko yanahitajika katika jeshi.



Kazi ya jeshi na MBR-200: 1982-1991 

 Miaka mitano baada ya kuianzisha ELPV, Chávez alianzisha mapambano mapya ya siri ndani ya jeshi, EBR-200, baadaye aliiboresha MBR-200. Akivutiwa na viongozi watatu wa Venezuela aliowahusudu sana, Ezequiel Zamora (1817-1860), Simon Bolivar (1783-1830) na Simon Rodriguez (1769-1854), watu hawa wa kihistoria walijulikana kama "mizizi mitatu ya mti" wa MBR-200.
 

Baadaye alielezea msingi wa kundi hilo, Chávez alisema kuwa na "mfumo wa Bolivarian ulioanzishwa haukuwa na malengo ya kisiasa... malengo yake yalikuwa ya ndani. Juhudi zake zilielekezwa katika mahali pa kwanza pa kujifunza historia ya jeshi la Venezuela kama chanzo chetu wenyewe cha mafundisho ya kijeshi, ambacho hakikuwepo."
 

Hata hivyo, alitumaini kwamba MBR-200 itatawala kisiasa, na mawazo yake kisiasa wakati huo, alisema kuwa "huu mti (wa Bolívar, Zamora na Rodríguez) unatakiwa kuwa mduara, unatakiwa kukubali kila aina ya mawazo, kutoka upande wa kulia, kutoka kushoto, kutoka mabaki ya kiitikadi ya wale wa zamani wa mifumo wa kibepari na kikomunusti."




No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...