Monday, November 12, 2012

DODOMA.



MKUTANO WA CCM TAIFA WAENDEA MJINI DODOMA

MWENYEKITI WA CCM TAIFA DOKTA JAKAYA MRISHO KIKWETE
Mkutano mkuu wa Chama Cha Mapinduzi CCM nchini umeanza mjini Dodoma na unatarajiwa kuendelea kwa siku tatu. 

Lengo la mkutano huo ni kuwachagua viongozi wa kitaifa wa chama hicho. 

Rais Jakaya Kikwete ambaye ndiye mwenyekiti taifa wa chama hicho anapigiwa upatu kuhifadhi wadhifa wake ingawa kumejitokeza fununu kwamba kuna baadhi ya wajumbe wanaopanga kuhujumu jitihada za kumrudishia rais Kikwete wadhifa wake. 

Vipeperushi ambavyo vilitawanywa katika maeneo mbalimbali ya mji wa Dodoma jana  vilikuwa na ujumbe unaosomeka: “CCM inayumba, kwa pamoja tumpunguzie mzigo mheshimiwa Rais kwa kumvua kofia moja ya uenyekiti, nina imani kwa pamoja tutashinda, piga kura ya hapana kwake, CCM oyeeee.”

-Haya ni Matokeo ya chaguzi za nafasi 10 za wajumbe wa NEC Tanzania Bara wa Chama cha Mapinduzi zinazoendela Dodoma yametoka ni kama ifuatavyo:


1.  Stephen Wassira                     - 2,135
2.  January Makamba                - 2,093
3.  Mwigulu Nchemba                - 1,967
4.  Martine Shigela                      - 1,824
5.  William Lukuvi                       - 1,805
6.  Bernard Membe                     - 1,455
7.  Mathayo David Mathayo   - 1,414
8.  Jackson Msome                     - 1,207
9.  Wilson Mukama                     - 1,174
10. Fenela Mukangara               -     984

No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...