Thursday, September 27, 2012



     JK. AWAAPISHA VIONGOZI WAKUU WA JESHI. 

Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania na amiri jeshi mkuu Dokta Jakaya Mrisho Kikwete amemwapisha mnadhimu mkuu wa jeshi la wananchi wa Tanzania JWTZ Luteni Jeneral Samuel Albart Ndomba.

Amiri jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama ,rais Jakaya mrisho Kikwete akimwapisha mnadhimu mkuu wa Jeshi la wananchi wa Tanzania Luteni Jenerali Samuel Albart Ndomba.

Katika hafla fupi iliyofanyiika jana katika viwanja vya ikulu jijini Dar es salaam rais Kikwete pia ameemwapisha mkuu wa jeshi la kujenga taifa  JKT  Meja Jenerali Raphael Mugoya Muhuga
 

Amiri jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama ,rais Jakaya mrisho Kikwete akimwapisha  mkuu wa jeshi la kujenga taifa JKT Meja Jenerali Raphael Mugoya Muhuga.

Luteni jeneral Ndomba ,aliyekuwa mkuu wa JKT ananchukuwa nafasi iliyoachwa wazi na Luteni Jeneral Abdulrahman A Shimbo ambaye amestaafu jeshi kwa mujibu wa sheria baada ya kufikisha umri wa miaka 60.

Meja Jeneral Raphael Mugoya Muhuga alikuwa mkuu wa utawala na mafunzo jeshi la kujenga taifa.

Amiri jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama ,rais Jakaya mrisho Kikwete Waziri mkuu Mizengo Pinda ,Waziri wa ulinzi na Jeshi la kujenga taifa Shamsi Vuai Nahodha ,Mkuu wa majeshi Jeneral Davis Mwamunyange katika picha ya pamoja  na viongozi wakuu wapya wa majeshi ya ulinzi na usalama.


No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...