Tuesday, September 18, 2012


Chama cha wanasheria Tanzania bara kimemtaka raisi wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania DK Jakaya kikwete kuchunguza baadhi ya tuhuma zinazowakabili baadhi  ya majaji katika mahakama mbali mbali nchini kufuatia tuhuma alizo zito mbunge Tundu Lissu katika bunge lililo pita 

Bunge la jamuhuri ya muungano wa Tanzania ni moja ya muhimili muhimu kwa maendeleo ya wananchi ambapo wabunge hukutana na kujadili masuala mbali mbali yanayo wahusu wananchi wao katika Nyanja mbali mbali ili kuyapitia ufumbuzi licha ya kuwa ndani ya mijadala hiyo mambo mengi huibuka zikiwemo kashfa na tuhumha kwa baadhi ya viongozi kama ambavyo katika bunge lililopita yaliweza kujitokezo

Miongoni mwa tuhuma zilizojitokeza katika msimu wa bunge uliopita ni pamoja alizo zitoa mbunge  wa singida mashariki ambaye ni mnadhimu mkuu wa  kambi rasmi ya upinzani bungeni Tundu Lissu kuwatuhumu baadhi ya majaji katika baadhi ya mahakama hapa kuwa wameteuliwa wakiwa hawana sifa zinzotakiwa kwa majaji 

 

Tanzania ni nchi ya kidemokrasia iliyopata uhuru tangu mwaka 1961 na ni nchi inayoaamika kuwa ni amani kutokana na historia yake na kila mwanachi ana haki ya kuishi na kwa mujibu wa ibara ya 26 ya katiba ya jamuhuri ya muungano kila mtu ana wajibu wa kutii na kuheshimu sheria za nchi.

No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...