Monday, October 29, 2012



DKT. MWAKYEMBE AZINDUA RASMI  USAFIRI WA TRENI YA ABIRIA DAR ES SALAAM. 
WAZIRI  WA UCHUKUZI DKT HARISON MWAKYEMBE AKIWAZINDUA HUDUMA YA USAFIRI WA TRENI KATIKA JIJI LA DAR ES SALAAM  ,KUSHOTO KWAKE  NI KAIMU MKURUGEZI TAZARA DAMAS D.NDUMBARO.
Wakati jiji la Dar es salaam likiwa ni miongoni mwa  miji inayoongoza duniani kwa  adha ya foleni barabarani ,sasa tatizo hilo limeanza  kupatiwa mwarobaini  baada ya serikali kuanzisha  usafiri  wa treni ya abiria .

Akizindua huduma hiyo jijini Dar es salaam Waziri Mwakyembe amesema  kuanza kwa safari hizo  ni hatua mojawapo  ya utatuzi wa  kero ya  usafiri jijini hapa  kero ambayo  imekuwa ikisababisha hasara ya mabilioni ya fedha   kila siku  kutokana na wafanyakazi kuchelewa kufika kazini kwa wakati .

Aidha waziri Mwakyembe amesema  kwa sasa milango iko wazi kwa wawekezaji wanaopenda  kuwekeza kwenye usafiri huo  na kwamba  tayari zabuni zimeanza kutangazwa.
BAADHI YA WAKAZI WA JIJI LA DAR ES SALAAM WAKIFURAHIA KUANZA KWA HUDUMA YA USAFIRI WA TRENI.
Amewaasa   wakazi wa jiji la Dar es salaam  kufuata utaratibu uliowekwa ikiwa ni pamoja   na kukata tiketi  wakati wa safari ambapo nauli  ni shilingi 400 na shilingi 100 kwa mwanafunzi.

Hii ni hatua  muhimu iliyofikiwa  na serikali  katika kuondoa kero ya foleni katika jiji la Dar es salaam ambapo miundombinu ya barabara zilizopo kwa sasa haikidhi idadi ya wakazi wake kwani ilijengwa wakati wa mkoloni Dar es salaam ikiwa na wakazi laki nne ambapo  kwa sasa idadi  inakaribia watu milioni tano .

-HABARI HII IMEANDIKWA NA  HILALI RUHUNDWA.


No comments:

Post a Comment

AddThis

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...