SEREKALI
YATAKIWA KUBOMOA NYUMBA YA MH. MCHUNGAJI
DOKTA GETRUDE PANGALILE LWAKATARE
Serikali imetakiwa,
kuibomoa nyumba ya Mbunge wa Viti Maalum kwa tiketi ya cha mapinduzi (CCM), Mchungaji Dokta Getrude Lwakatare.
Nyumba ya mchungaji Dokta Getrude Lwakatare. |
Akitoa taarifa kwa vyombo siku ya jumapili Waziri Kivuli, Wizara ya Ardhi,
Nyumba na Maendeleo ya Makazi ambaye pia ni Mbunge wa Kawe (CHADEMA), Halima
Mdee.amesema kuwa wakati raia wengine wakibomolewa nyumba kama ilivyo ya
Mchungaji Lwakatare, zilijengwa kinyume cha sheria
Mdee alisema wakati kigogo huyo (Lwakatare) amehamia kwenye nyumba yake katika, mto Ndumbwi, bahari na mazingira kwa ujumla yameharibiwa, lakini zaidi kuwepo raia waliobomolewa kwa mujibu wa sheria hizo.
Mdee alinukuu Sheria ya Mazingira, sura 191 ya mwaka 2004, fungu 57(1), inasema hairuhusiwi kufanya shughuli zozote za kudumu za kibinadamu ndani ya mita 60.
Operesheni ambayo ilihusisha takriban nyumba 15 na kuta nane. Lakini kinachoelezewa kuwa ni kizungu mkuti nyumba ya Mchungaji Lwakatare haikuguswa.
Hata hivyo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Dk Terezya Huvisa, aliwahi kuwaambia waandishi wa habari mjini Dodoma kuwa, nyumba hiyo haikubomolewa kutokana na pingamizi la mahakama.
Nyumba inayotajwa kuwa mali ya Mchungaji Lwakatare, imejengwa kwenye viwanja namba 2019-2020 Kawe Beach, katika fukwe za bahari ya Hindi.
No comments:
Post a Comment