MICHELLE OBAMA AMTETEA MUMEWE KATIKA KINYANYANYIRO
Mke wa rais wa Marakeni Barack
Obama, Michelle Obama amemuunga mkono mumewe katika mkutano mkuu wa chama cha
Democratic akiomba rais huyo apewe muda zaidi.
Bibi Obama amekiri kuwa mabadiliko
ambayo mumewe Barack Obama aliahidi wakati wa kampeini ya wadhifa wa urais
miaka minne iliyopita hayajatimizwa kikamilifu lakini akawaomba wapiga kura
kumpa miaka mingine minne ili kuuimarisha uchumi wa Marekani unaoyumbayumba.
Michelle Obama ndiye aliyekuwa wa
kwanza kumtetea mumewe katika siku ya kwanza ya mkutano huo wa siku tatu ambao
utakamilika kwa hotuba ya Obama kesho Alhamisi ili kukubali uteuzi wa chama cha
Democratic wa kupambana na Mitt Romney katika uchaguzi wa uraisi tarehe sita
Novemba.
Bi Obama alisema "Kama rais, utapata ushauri wa kila
aina kutoka kwa watu tofauti, lakini unapohitajika kufanya uamuzi wako kama
rais, kinachokuongoza ni maadili na maono yako pamoja na uzoefu wa maisha,
mambo yanayokufanya uwe jinsi ulivyo"
Katika kinyang'anyiro ambacho ni
kikali kutabiri zikiwa zimebaki wiki tisa kabla ya Wamerakani kupiga kura,
Obama anakabiliwa na upinzani mkali kutoka kwa mgombea wa Republican Mitt
Romney kwa sababu ya kudorora uchumi pamoja na asilimia 8.3 ya ukosefu wa
ajira.
Rais huyo anajaribu kutumia mkutano
huu mkuu kufufua tena msisimko uliombeba hadi katika ushindi wa mwaka wa 2008
lakini akakiri kwa mwaandishi wa habari mmoja wa televisheni ya Colorado kuwa
hajatimiza alicholenga kufanya katika muhula wa kwanza.
Michelle Obama amesema na hapa
namnukulu “kwa Barack, mafanikio siyo kiasi cha pesa ambacho unapata, ni kuhusu
tofauti unayoweka katika maisha ya watu.” Wazungumzaji katika kongamano hilo
walimshambulia Romney kuhusu rekodi yake ya kibiashara, kukataa kulipa kodi
zaidi na kwa kuongoza vita vya Warepublican dhidi ya wanawake.
No comments:
Post a Comment